Kijiji cha Makiba chenye vitongoji 4 ambavyo ni Songambele,Makiba,Korona na Mtoni,vitongoji vyote hivi vyenye jumla ya idadi ya watu wasiopungua Elfu 3 kina Mradi mmoja wa Maji ya kisima ambao una vituo vichache vya kuchotea Maji , jambo ambalo limekua changamoto ya upatikanaji wa Maji katia kijiji hicho.Haya yamedhihirika kwenye mkutano wa Hadhara wa wananchi wa kijiji hicho walipopokea kwa furaha Utambulisho wa Mradi Mpya wa usambazaji maji kama inavyolekeza Sera ya maji ya 2002 kuwataka wananchi kushiriki katika uibuaji wa miradi ya Maji.
Akizungumza kwenye mkutano huo mwenyekiti wa kijiji hicho Joseph Adamu ameeleza kua baadhi ya wanakijiji wameshindwa kuhudhuria mkutano huo kutoka na shughuli mbali mbali kuingiliana pia Ameishukuru Halmashauri ya Meru kwa kupeleka mitambo yake katika kijiji hicho iliyotengeneza tuta la kuzuia maji yaliyokua adha kubwa kwa kusababisha mafuriko kipindi cha mvua katika Shule ya Sekondari Makiba akitia msisitizo kwa kumweleza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Kristopher J. Kazeri " Mkurugenzi hii ndio maana ya huduma kwa wananchi "
Wananchi hao wametoa mapendekezo mbali mbali ikiwemo vitongoji vyote kupata maji kwani yaliyopo hayatoshelezi pia wame lalamikia la bei ya Maji kuwa juu kulinganisha na hali zao za kiuchumi Naye Mwandisi wa Halmashauri hiyo Happy Mrisho amepokea maoni ya wananchi hapo pia amesema kuhusu upatikanaji wa maji katika mradi mpya wataainisha na vituo kwaajili ya kunweshea mifugo kwani jamii ya watu wa Makiba ina wafugaji pamoja na kuweka vituo vya kuchotea maji vya kutosha kwa umbali wa miata 400
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa