Wamiliki wa shule binafsi wilayani Arumeru wamepewa siku hamsini kuanzia tarehe 26.05.2017 mpaka 15.07.2017 kuhakikisha wanalipa madeni yao ya kodi wanazodaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania 'TRA'.
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Alexander Mnyeti alipokutana na wamiliki wa shule binafsi za msingi na sekondari zinazoendeshwa katika wilaya ya Arumeru alipokutana nao kwenye ukumbi wa mikutano Halmashauri ya Meru.
Mkuu wa wilaya Mnyeti amesema amelazimika kuwaita baada ya kufuatilia na kuona shule nyingi binafsi hazilipi kodi ya serikali kwa kivuli cha kuwa wanatoa huduma.
"Ninyi wamiliki wa shule hamlipi kodi ya serikali kwa kivuli cha kutoa huduma lakini nimefanya utafiti na kugundua mnatoza ada kubwa kati ya milioni moja na nusu mpaka milioni tatu kifupi hiyo ni biashara sio huduma" alisisitiza Mnyeti. Mnyeti amewaelekeza wamiliki wa shule hizo binafsi kuwa shule inayotoa huduma mwanafunzi anatakiwa kulipa ada elekezi ya serikali ya shilingi elfu sabini na tano kama shule za serikali zinavyofanya laini hakuna shule binafsi inayofanya hivyo. Aidha Mnyeti amefafanua kuwa kodi zinazotakiwa kulipwa TRA na shule hizo ni kodi inayokatwa kwenye mishahara ya watumishi waliojiriwa pamojana kodi ya mapato baada ya kupata faida ya biashara iliyofanyika.
"Katika siku hamsini nilizotoa ni fursa ya mmiliki wa shule kwenda TRA kufahamu kiasi cha kodi anachodiwa na kujipanga namna ya kulipa" ameshauri Mkuu wa Wilaya huyo.
Ingawa baadhi ya wamiliki wa shule hizo kulalamikia kutokupata faida katika uendeshaji wa shule zao lakini Mkuu wa wilaya alihoji mbona shule hizo hazifungwi kama hakuna faida.
"Haiwezekani kuendesha biashara miaka nenda rudi na useme haina faida bila kufunga biashara hiyo, wazazi wanalipa mamilioni ya mapesa hivyo ni lazima serikali ipate halali yake kupitia Kodi" alisisitiza zaidi Mnyeti
Hata hivyo baadhi ya wamiliki wa shule hizo waliridhika na ulipaji wa kodi ya mapato na kukubaliana kwa pamoja kuridhika na muda huo waliopewa kukamilisha ulipaji wa kodi ya mapato
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa