Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amepongeza ujenzi wa vyumba vitatu (3) vya Madarasa na ofisi ya Walimu Katika Shule ya Sekondari Umoja King'ori ambapo amewataka kuhakikisha wanapaua majengo hayo kwa wakati.
Mwl.Makwinya amesema ni muhimu kutumia mbao zilizopo kwa wakati Ili kuleta tija zaidi kwenye miradi hiyo.
Nae Diwani wa Kata ya King'ori Mhe.Lucas Kaaya ameishukuru Halmashauri kutoa mbao za kupaua vyumba hivyo ambapo ameahidi kushirikiana na Wananchi na wadau mbalimbali kupaua Madarasa hayo mapema .
Kata ya King'ori ni Miongoni mwa Kata saba ambazo Mkurugenzi Zainabu amefanya ziara ya kukagua na kutembelea utekelezaji wa miradi ya EP4R ,Miradi ya Nguvu za wananchi na michango ya wahisani,miradi ya TASAF pamoja na maboma ya mda mrefu ,ambapo aliambatana na Afisa Elimu Sekondari pamoja na Wahandisi wa Ujenzi toka Halmashauri.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa