Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mheshimiwa Jerry Muro, anawatangazia wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kushiriki mbio za Mwenge wa Uhuru 2019, utakaowasili kesho tarehe 09.06.2019, kwenye Halmashauri ya Meru kutoka Halmashauri ya Arusha Vijijini.
Katika Halmashauri ya Meru, Mwenge wa Uhuru 2019, utapokelewa saa 02:00 asubuhi, kwenye viwanja vya Peace point kata ya Ambureni.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2019, Ndugu Mzee Mkongea Ali, atakimbiza Mwenge wa Uhuru umbali wa Kilomita 122.2 na kukagua jumla ya miradi 8, yenye thamani ya shilingi bilioni 7,005,350,943.50 miradi iliyolenga sekta ya Maji, Elimu, Afya, Mazingira, Mifugo na Viwanda.
Wananchi wote mnaombwa kushiriki mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 kwenye maeneo ya Miradi ya Maendeleo na baadaye kwenye sherehe za mkesha zitakazofanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Muungano Kata ya Usa -River
Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2019" Maji ni Haki ya Kila mtu, tutunze vyanzo vyake na Tukumbuke kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa"
Burudani mbalimbali zitakuwepo kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa