Mkuu Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango ametoa siku 14 kwa wote waliovaamia Shamba la Valeska lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Meru kupisha taratibu za kitaalamu katika Shamba hilo ambalo awali lilikuwa likimilikiwa na Arusha Cooperative union limited (ACU) , ambapo Mwaka 2008 Serikali ilifuta umiliki wake kutokana na ACU kushindwa kuliendeleza .
Mhe. Ruyango ametoa agizo hilo baada ya kuzungumza na wananchi wa Vijiji Vitatu vinavyozunguka Shamba hilo vya Maroroni, kwaugoro na Valeska ambavyo kila kimoja kimepewa Ekari 500 kutoka Shamba hilo lenye ukubwa wa Ekari 4087 lililofutiwa umiliki na Serikali kwa maslahi mapana ya taifa, ambapo Halmashauri ya Meru ilipewa jukumu la kuligawanya kwa kuzingatia maelekezo yaliyotolewa.
Kesia Kaaya ambaye ni mkazi wa kijiji Cha Valeska ameishukuru Serikali kwa kutoa Ekari 500 kwani zitasaidia kupunguza uhitaji wa Ardhi "japo Ekari 500 hazitoshi tunaishukuru Serikali kwani tunachangamoto ya ufinyu wa Ardhi, wengi hatuna makazi pia tunaitaji maeneo ya huduma za jamii na ardhi ya vijana kujiajiri kwenye kilimo cha mbogamboga "amesema Kesia
Nao Wananchi waliovaamia Shamba hilo kwa kujishughulisha na kilimo cha mbogamboga wamesema hawana budi kufuata maagizo ya Serikali japo hawakutarajia kuondolewa kwa muda uliotolewa "kwa sasa najishughulisha na kilimo cha pilipili katika Shamba hili" amesema Reward Komba
Nao Waheshimiwa Madiwani wa Kata ya Maroroni na Makiba, ambao Kata zao zina Vijiji vilivyopewa Ekari 500 wametoa wito kwa Wananchi kuwa watulivu wakati taratibu za kitaalum ikiwemo upimaji zikiendelea katika Shamba hilo
Ikumbukwe, tarehe Mosi Julai 2021 Mhe.Wilium Lukuvi Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alifanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru na kutoa maelekezo ya Serikali juu ya upangaji wa Shamba la Valeska ikiwa ni pamoja na kuelekeza Vijiji Vitatu vinavyozunguka Shamba Hilo kupewa Ekari 1,500 kwa mgawanyo wa Ekari 500 kwa kila kijiji.
Baadhi ya picha za tukio.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango akizungumza na Wanakijiji wa Kijiji cha Maroroni na kwaUgoro.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Mwl.Zainabu Makwinya wakati wa Ziara ya Mhe.Mkuu wa Wilaya Kata ya Maroroni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru akizungumza na wananchi wa Maroroni.
Baadhi ya Wanakijiji wa Kijiji chaValeska wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Kijiji chaValeska wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Kijiji chaValeska wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Vijiji vya Maroroni na kwaugoro wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Vijiji vya Maroroni na kwaugoro wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Vijiji vya Maroroni na kwaugoro wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Vijiji vya Maroroni na kwaugoro wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Baadhi ya Wanakijiji wa Vijiji vya Maroroni na kwaugoro wakifuatilia Mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa