Halmashauri ya Wilaya ya Meru imefanya kikao cha tathmini ya lishe kwa kipindi cha mwezi Julai-Septemba 2023 kwa mwaka wa Fedha 2023/2024.
Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo kwa lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Lishe.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kikão hicho, Mkuu wa Wilayaya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda ameeleza kuwa suala la Lishe lichukuliwe kwa uzito mkubwa kwani bila kuwa na Taifa lenye Afya bora hatuwezi kuwa na maendeleo.
" Bila kuwa na wananchi wenye afya bora hatuwezi kuwa na maendeleo ya Nchi yetu kwani maendeleo yanatatutwa na watu wenye nguvu na afya" Alisema Kaganda.
Rehema Lema ni Afisa Lishe Halmashauri ya Meru amewasilisha taarifa ya shughuli za Lishe ikiwa ni pamoja na kufuatilia utekelezaji wa mkataba wa Lishengazi ya Kata na Vijiji, Ufuatiliaji wa ukuaji wa watoto chini ya miaka mitano, utoaji wa vidonge(FEFO) vya kuongeza damu kwa wajawazito, Utoaji wa matone ya vitamin A na dawa za Minyoo, unyonyeshaji wa watoto wachanga pamoja na maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe Kijiji (SALIKI).
Aidha, Mhe. Kaganda ametoa Maelekezo kwa Afisa Lishe na Watendaji wa Kata zote 26 katika Halmashauri ya Meru kuweka Utaratibu wa kutoa elimu ya Lishe katika maeneo yao.
" Tuongeze wigo wa kutoa elimu ya lishe Makanisani, Msikitini, shuleni na hata kwenye vikao vya kimila ili nao wawe sehemu ya kusambaza elimu lishe kwenye jamii." alisema Mkuu huyo.
Hata hivyo, Mhe. Kaganda ametoa Pongezi kwa Afisa Lishe kwa utoaji wa elimu ya lishe katika Kata ya Ngabobo.
Pia, Pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji Mwl. Zainabu J. Makwinya kwa kuwezesha vikao vya lishe kufanyika.
Vilevile, Mhe. Kaganda amewakumbusha Watendaji wa Kata kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo yao kuhusu kutumia mvua hizi zinazoendela kunyesha kupanda mazao ya muda mfupi.
Ikumbukwe kuwa Lishe ni sehemu ya utekelezaji Wa llani ya chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 Sura ya 3 Ibara ya 85 ambapo imeelezwa umuhimu wa Lishe "Lishe bora ni muhimu katika kuhakikisha Taifa linakuwa na jamii yenye nguvu kazi imara na uwezo mkubwa wakuelewa na kukabiliana na mazingira yake".
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa