Katibu tawala Wilaya ya Arumeru Mwl.James Mchembe ameipongeza Taasisi ya maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD) kwa Kushirikiana na Idara ya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Meru kufanya matembezi ya hisani ya kuhamasisha jamii kujikinga na maambukizi ya Uviko-19 ambayo yameambatana na utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 ,Elimu juu ya magonjwa yasioambukiza na uchangiaji damu.
Akizungumza na hadhara ya Wananchi eneo la Hospital ya Wilaya ya Meru,Mwl. Mchembe ametoa wito kwa wadau wengine kuungana na Serikali kwenye mapambano dhidi ya UVIKO-19 kwa kuhamasisha jamii kupata chanjo"Serikali imehakikisha chanjo ya UVIKO-19 inapatikana, nitoe wito kwa Wananchi kupata Chanjo .
Vilevile Mwl Mchembe ametoa rai kwa vijana kuwa mstari wa mbele kupata chanjo hiyo sambamba na kuwa mabalozi wa kuisemea vyema chanjo hiyo.Pia ametoa wito kwa wadau wengine kuiga taasisi ya TICD.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Meru Dkt Maneno Focus amesema Halmashauri hiyo imehakikisha inawafikia Wananchi kwenye maeneo yao kwa kuendesha zoezi la chanjo nyumba kwa nyumba,taasisi za Elimu na dini.Ambapo dozi 4560 Sawa na asilimila 76 % ya Chanjo zilizopokelewa awamu ya pili zimetolewa kama dozi ya kwanza na utoaji wa dozi ya pili unaendelea.
Aidha Dkt.Focus ametoa wito kwa jamii kupata Chanjo ya UVIKO-19 ambapo ameainisha kuwa chanjo aina ya Pfizer imepokelewa na itapatikana katika vituo vyote vya kutolewa huduma.
Naye ,Mkuu wa TICD Tengeru Dkt.Bakari Juma amesema katika kuadhimisha wiki ya maendeleo ya Jamii wamefanya matembezi ya hisani kuunga mkono Juhudi za Mhe.Rais katika mapambano dhidi ya Uviko-19.
Mhe.Juliasi Mungure ambaye ni Diwani wa Kata ya Akheri ametoa wito kwa Wananchi kupata Chanjo kwani Serikali imeendelea kuhakikisha wanakuwa salama kwa kuleta chanjo hiyo.
Mwl.James Mchembe akizungumza baada ya matembezi ya hisani kuhamasisha chanjo ya UVIKO-19
Dkt.Bakari George akizungumza baada ya matembezi ya hisani kuhamasisha chanjo ya UVIKO-19
Mhe.Julias Mungure akizungumza baada ya matembezi ya hisani kuhamasisha chanjo ya UVIKO-19
Dkt.Maneno Focus akizungumza baada ya matembezi ya hisani kuhamasisha chanjo ya UVIKO-19
Picha ya pamoja Meza Kuu na Wanafunzi wa TICD
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa