Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango ametoa wito wa wahitimu wa Operasheni maalum ya Samia Suluhu Hassan Kutumia Mafunzo hayo kwa tija kwani Serikali imetumia gharama kubwa kuhakikisha Mafunzo hayo yanafanyika.
Mhandisi Ruyango amesema hayo wakati wa kufungua Mafunzo ya Operasheni maalum ya Samia Suluhu Hassan katika kikosi Cha JKT Oljoro yaliyofanyika kwa muda wa Miezi mitatu ambapo ametoa wito kwa wahitimu hao kujikinga na ugonjwa wa UVIKO 19 "Taifa linawategemea Vijana, mlipokuwa kambini mlikuwa salama kwa sasa mnakwenda kuchangamana na watu mbalimbali ni vyema kuendelea kuchukua tafadhari ikiwa ni pamoja na kupata chanjo "Amehimiza Ruyango.
Mwakilishi wa Mkuu wa JKT kanali Amos Mollo ambaye pia ni Mkurugenzi Operasheni na Mafunzo Makao Makuu ya JKT ametoa wito kwa vijana kuona haja ya kujiunga na mafunzo ya JKT kwani yanalenga kuwajengea uimara, uhodari na uzalendo wa kulitumikia Taifa pamoja na ujasiri.
Aidha, Kanali Mollo amewataka wahitimu hao kujilinda dhidi ya maradhi mbalimbali yakiwemo maradhi yanayosababishwa na tabia pamoja na ulaji sambamba .
Aidha, miongoni mwa changamoto zilizo ainishwa katika risala ya wahitimu hao ni pamoja na ratiba ya udahili wa chuo na bodi ya mikopo ambapo wameiomba Serikali kuona namna ya kuongeza muda wa Mafunzo kuwa Miezi 6.
Ikumbukwe katika kuhakikisha kazi na shughuli mbalimbali zinaendelea mbali na uwepo wa Janga la UVIKO 19, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alitoa fursa ya kuwepo kwa Mafunzo ya JKT ambapo katika kambi ya Oljoro wahitimu 2190 wamehitima mafunzo hayo wakiwemo Wasichana 518 na wavulana 1672.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango akizungumza
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akikagua gwaride la wahitimu Operasheni ya Samia Suluhu Hassan.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru na Viongozi wa JKT.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ,Viongozi wa JKT na Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Arumeru.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Viongozi wa JKT na wahitimu wa Operasheni maalum ya Samia Suluhu Hassan.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa