• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Elimu Sekondari

Sekta ya Elimu Sekondari

Halmashauri ya Wilaya ya Meru ina jumla ya shule 57 za Sekondari, kati ya hizo Shule 29 zinamilikiwa na Serikali na Shule 28 zinamilikiwa na taasisi zisizo za Serikali. Katika shule 29 za serikali, shule tatu (3) zina kidato cha Tano na Sita ambazo ni Maji ya Chai, Kisimiri na Makiba.

Aidha shule zisizokuwa za serikali zenye kidato cha Tano na Sita ni pamoja na St.Mary’s Duluti, Makumira, Mariado, Usa River Seminary, Ailanga, Star High school, Ngarenanyuki, Tanzania Adventist, Hebron na Jude Moshono.

1.1 Idadi ya Walimu

Halmashauri ya Wilaya ya Meru ina jumla ya walimu 1,318 katika shule za Sekondari za serikali kwa takwimu za Mei, 2017 kwa mchanganuo ufuatao:-

Jedwali Na. 1: Mahitaji ya walimu kwa masomo

MASOMO
MAHITAJI
WALIOPO
UPUNGUFU
ZIADA
Sayansi na Hisabati
204
139
65
0
Biashara
24
12
12
0
Sayansi ya Jamii
705
1155
00
450
Jumla
910
1,318
77
450

 

Aidha mwezi APRIL 2017 Serikali iliajiri walimu wapya wa Sayansi na Hisabati ambapo Halmashauri ilipangiwa walimu 11 kati ya hao walimu 10 wameripoti vituoni na tayari wameanza kazi.

1.2 Uandikishaji Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza 2017

Jumla ya wanafunzi 4,352 (wavulana 1964, wasichana 2,388) wamechaguliwa kuanza kidato cha kwanza mwaka 2017. Hadi tarehe 17 Mei, 2017 wanafunzi ambao wamekwisha kuripoti shuleni ni wanafunzi 3,551 (Wavulana 1572 na wasichana 1979) ambao ni sawa na 84% ya wanafunzi wote waliochaguliwa.

Aidha kulikuwa na changamoto katika kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza, ikiwemo upungufu wa madarasa, viti na meza. Hatua zilizochukuliwa katika kukabiliana na changamoto tajwa ni pamoja na kutumia Tsh.62,492,300 za mapato ya ndani kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 15 kwenye shule zenye upungufu. Pia kiasi cha Tsh.19,684,384 kutoka mapato ya ndani kimetumika kwa ajili ya kununua meza/viti 328 kwa ajili ya wanafunzi.

1.3 Mahitaji ya Miundo Mbinu

Mahitaji ya Miundombinu ya elimu ambayo ni vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, ofisi, vyoo vya wanafunzi na walimu ni kama yanavyoonekana hapo chini.

Jedwali Na. 2: Miundombinu ya shule za sekondari.

Aina ya Miundo Mbinu
Mahitaji
Yaliyopo
Upungufu
Maabara

87

56

31

Nyumba za Walimu

910

96

814

Jengo la Utawala

29

19

10

Vyumba vya Madarasa

361

319

42

Matundu ya Vyoo.

613

392

221

Maktaba

29

5

24

 

1.4 Meza na Viti vya wanafunzi

Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa sasa ina idadi ya wanafunzi 11,736 hivyo kufanya mahitaji ya meza na viti kuwa11,736. Aidha kuna baadhi ya shule ndani ya Halmashauri zina upungufu wa viti 935 na meza 786 lakini pia kuna baadhi ya shule ndani ya Halmashauri zina ziada ya viti 2,185 na meza 1,892. Shule hizi zipo katika kata tofauti tofauti hivyo ni changamoto kuhamisha viti au meza kutoka shule moja kwenda shule nyingine kwa kuwa samani hizi zilitengenezwa kwa nguvu ya jamii za kata husika. Ili kukabiliana na changamoto hii viti/meza za ziada zimehamishwa kutoka shule zenye utoshelevu kwenda kwenye shule zenye upungufu.

Jedwali Na. 3

Idadi ya Shule

29

Idadi ya Wanafunzi

11,736

Idadi ya Samani
MAHITAJI
YALIYOPO
UPUNGUFU
ZIDIA
VITI
MEZA
VITI
MEZA
VITI
MEZA
VITI
MEZA
11736
11736
12986
12945
935
786
2185
1892

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

1.4 TAARIFA YA KINA KUHUSU MIRADI YA ELIMU SEKONDARI

Jedwali Na.4

S/N 

AINA YA MRADI

MAHALI ULIPO

MWAKA ULIPOANZA

GHARAMA ZA MRADI

WAHUSIKA WA GHARAMA

JINA LA MRADI
GHARAMA ZA KUKAMILISHA
HATUA YA MRADI 
WANUFAIKA

1

UJENZI WA MADARASA 2, NYUMBA MOJA YA WALIMU (SIX IN ONE) MATUNDU MAWILI(2 STANCES) NA MATUNDU MANANE YA WANFUNZI ( 8 STANCES)

MALULA SEKONDARI

2014/15

221,637,000

WORLD BANK

MMES II
221,637,000
MRADI ULIKAMILIKA
WANAFUNZI 80 WALIMU SITA NA WANAFUNZI 331 WA SEKONDARI MALULA 

2

UJENZI WA MADARASA 2, NYUMBA MOJA YA WALIMU (SIX IN ONE) MATUNDU MAWILI(2 STANCES) NA MATUNDU MANANE YA WANAFUNZI ( 8 STANCES

MOMELA SEKONDARI

2014/15

222,000,000

WORLD BANK

MMES II
222,000,000
MRADI ULIKAMILIKA
WANAFUNZI 80 WALIMU SITA NA WANAFUNZI 387 WA SEKONDARI MOMELA

3

UJENZI WA MATUNDU 8 YA VYOO VYA WANAFUNZI ( 8 STANCES) NA MATUNDU MAWILI YA WALIMU( 2 STANCES)

KITEFU

2014/15

20,000,000

WORLD BANK

MMES II
20,000,000
MRADI ULIKAMILIKA
WANAFUNZI 240 NA WALIMU 42 WA SHULE YA SEKONDARI KITEFU

4

UJENZI WA MADARASA MAWLI ( 2 CLASSROOMS) MATUNDU 8 YA VYOO VYA WANAFUNZI ( 8 STANCES)

LAKITATU SEKONDARI

2014/15

64,423,500

WORLD BANK

MMES II
64,423,500.00
MRADI UMEKAMILIKA
WANAFUNZI 275 WA SHULE YA SEKONDARI LAKITATU.

5

UJENZI WA MATUNDU MAWILI YA VYOO VYA WALIMU

POLI SEKNDARI

2016/17

4,907,654.47

WORLD BANK

P4R
4,907,654.47
MRADI UKO KATIKA HATUA YA UKAMILISHAJI
WALIMU 45 WA SHULE YA SEKONDARI

6

KUKAMILISHA MIUNDO MBINU YA MAABARA MOJA

SAKILA SEKONDARI

2016/17

6,756,379.60

WORLD BANK

P4R
6,756,379.60
MRADIUMEKAMILIKA
WALIMU 45 WA SHULE YA SEKONDARI

7

KUKAMILISHA MIUNDO MBINU YA MAABARA MOJA

LAKI TATU SEKONDARI

2016/2017

6,500,000.00

WORLD BANK
P4R
6,500,000.00
MRADI UKO KATIKA HATUA YA UKAMILISHAJI
WANAFUNZI 241 PAMOJA NA WALIMU 38

8

KUKAMILISHA VYUMBA VIWILI VYA MADARASA

NKOANEKOLI SEKONDARI

2016/2017

11,000,000.00

WORLD BANK

P4R
11,000,000.00
MRADI UKO KATIKA HATUA YA UKAMILISHAJI
WANAFUNZI 178 WA SHULE YA SEKONDARI MIRIRINI

9

UJENZI WA MATUNDU 8 VYOO VYA WANAFUNZI

MIRIRINI SEKONDARI

2015/2016

22,284,600

WORLD BANK

P4R
22,284,600.00
MRADI UMEKAMILIKA
WANAFUNZI 106 WA SHULE YA SEKONDARI NKOANEKOLI

10

UJENZI WA MABWENI 2,VYUMBA VYA MADARASA 8 NA MATUNDU 20 YA VYOO VYA WANAFUNZI.

KISIMIRI SEKONDARI

2016/17

480,000,000.00

WORLD BANK

P4R
480,000,000.00
MRADI UMEKAMILIKA.
 

1.6 Taaluma na Ufaulu

Kulingana na takwimu za Baraza la mitihani Tanzania (NECTA), ufaulu wa kidato cha nne (CSEE) kwa miaka mitatu iliyopita ni kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini.

 

Jedwali Na. 6: Ufaulu wa Kidato cha nne kuanzia mwaka 2013 hadi 2016

S/N

Mwaka

% ya Ufaulu

1

2016

76.23

2

2015

71.07

3

2014

74.32

4

2013

53.76

Aidha mtihani wa kidato cha sita (ACSEE) asilimia ya ufaulu (Daraja la I, hadi IV) kwa mujibu wa tathmini ya matokeo ni kama ifuatavyo

Jedwali Na. 5: Ufaulu wa Kidato cha sita kuanzia mwaka 2014 hadi 2016

S/N

Mwaka

% ya Ufaulu

1

2016

93.4

2

2015

99.6

3

2014

99.3

Katika mitihani ya kitaifa mwaka 2016 Halmashauri ya Meru imeshika nafasi mbalimbali kama inavyoonekana kwenye Jedwali lifuatalo.

 

Jedwali Na. 6: Nafasi za Kimkoa na Kitaifa

Kidato 
Nafasi Kimkoa
Nafasi Kitaifa
Kidato cha II

01

06

Kidato cha IV

01

19

Kidato cha VI
Shule ya Kisimiri ilikuwa ya Kwanza Kitaifa

Katika kuhakikisha ufaulu unafikia asilimia 80 kwa kidato cha nne kama ilivyoainishwa kwenye Mpango wa Matokeo Makubwa sasa - BRN, Halmashauri inafanya jitihada mbalilmbali. Miongoni mwa jitihada zinazochukuliwa ni kurekebisha ikama kwa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati, kutoa motisha kwa walimu kwa shule zitakazofanya vizuri kitaifa, kukamilisha ujenzi wa maabara za sayansi pamoja na kusimamia na kufuatilia kwa karibu ufundishaji shuleni.

1.7 Mpango wa Chakula

Shule zote 29 zimekuwa zikiendesha mpango wa chakula ambapo wazazi/walezi wanachangia huduma hiyo. Tangu utaratibu wa elimu bure kuanza huduma hii imekuwa haitolewi kwa ufanisi kwa kuwa baadhi ya wazazi wanaamini kuwa huduma hiyo inapaswa kutolewa bure. Shule zimehimizwa kupitia vikao vya bodi na wazazi kuhamasisha wazazi na kutoa elimu toshelevu kuhusu waraka wa elimu bure ili kukubaliana kwa kupitia mijadala ya wazi namna ya kuchangia huduma ya chakula kwa kuomba vibali Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pale ambapo huduma hiyo inahitaji mchango wa fedha.

1.8 CHANGAMOTO.

Zifuatazo ni baadhi ya changamoto zinazoikabili elimu ya sekondari katika Halmashauri ya Meru:-

S/N
CHANGAMOTO
MKAKATI WA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO.
1
Upungufu wa walimu Sayansi/Hisabati hivyo masomo hayo kutofundishwa ipasavyo.
Halmashauri imewasilisha mahitaji ya walimu hao wa sayansi TAMISEMI, kwa mwaka 2016/17 walimu 10 wameajiriwa.Shule zinahimizwa kushirikiana na wazazi kuchangia kuwalipa walimu wa sayansi na Hisabati wanaoajiliwa kwa muda ili kukabili uhaba.
2
Upungufu wa nyumba za walimu hasa kwa shule zilizoko pembezoni mfano Maruvango,Miririny,Mbuguni Makiba.
Bodi za shule na jamii zinahimizwa kutafuta wahisani wa kuchangia ujenzi wa nyumba za walimu.
Aidha jamii inahimizwa kuwatafutia walimu nyumba za kupanga zilizo jirani na shule.
3
Kusuasua kwa huduma ya chakula cha mchana kwa sababu ya uelewa usio sahihi kuhusu wajibu wa wazazi kuendelea kuchangia huduma ya chakula kwa shule za kutwa.
Kutoa elimu kwa wazazi kupitia vikao vyao na kuomba vibali vya kuchangia ofisi ya katibu tawala mkoa.
4
Upungufu wa majengo ya utawala (administration blocks) unaosababisha shule 21 kutumia vyumba vya madarasa kama majengo ya utawala.
Upungufu wa samani za ofisi unaosababisha walimu kutumia viti na meza wanafunzi.
Vipaumbele vya ujenzi vielekezwe kwenye ujenzi wa ofisi za shule na shule zitenge fedha kidogo kidogo kwenye fedha za elimu bure kwa ajili ya kununua samani za ofisi.
5
Wanafunzi wa kidato cha kwanza kutoripoti kwa wakati na wengine kuhamia shule zenye hosteli/bweni za Halmashauri nyingine za mkoa huu na nje ya mkoa au kwenda shule binafsi hivyo lengo la uandikishaji kutofikiwa kwa 100%.
Watendaji wa kata,maafisa elimu kata kuendelea kufuatilia walipo na hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi ya wazazi wanaozembea kuwaleta watoto wao shule.
Ujenzi wa mabweni au hosteli upewe kipaumbele kwenye mipango ya ujenzi wa miundo mbinu ya shule.

 

 

 

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa