• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UWEPO WA MDUDU MWARIBIFU WA ZAO LA MAHINDI MERU.

Imewekwa: March 23rd, 2018

Wakulima kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Meru washauriwa kuepuka hasara kwa kutembele na kukagua mazao kwenye  mashamba  yao mara kwa mara ili kubaini na kumdhibiti kwa wakati  mdudu mwaribifu aitwae kiwavijeshi kivaamizi (FALL AMRYWORM) anayeshambulia mimea ya aina 80 mbalimbali kama vile Mahindi,Mtama,Mpunga na uwele .

Akitoa Mafunzo kwa Wakulima wa kijiji cha Nkoasenga Afisa Kilimo Eliudi Saoyo  amesema  Mdudu huyo Mwaribifu asipo dhibitiwa kwa wakati huwa na Madhara makubwa kwani uharibifu wake huenda kwa hatua kwani huanza kuaribu mmea kwa kushambulia eneo la pembeni la jani na hatua ya pili hushambulia mmea kwa kutoboa jani huku hatua inayofuata ambayo ni vigumu kumdibiti kwani huingia ndani ya mmea ambapo hujitengenezea utando wa kujingika na viatilifu.

Aidha Saoyo amewashauri wakulima hao kuepuka hasara kwa kukagu mashamba yao mara moja na kumdhibiti  mdudu huyu kiwavijeshi kivaamizi  kwa kutumia  kiuatilifu (DAWA) pale wanapo baini uwepo wake  pia kutoa taarifa kwa wataalamu wakilimo ili kupata ushauri,

Afisa kilimo Saoyo amesisitiza kuwa matumizi ya viuatilifu ( dawa) hizoo lazima zizingatie vipimo sahihi kwani vipimo visipozingatiwa mdudu huyo hatokufa na kushauri aina ya viuatilifu vinavyoweza kutumika kuwa ni Duduba, Vaashield, Dasban, Duduall, Karate ,Selectroni, Abamecting.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nkoasenga Sifael K.Pallangyo  ambaye ni miongoni mwa wakulima wa mahindi ambao mashamba yao yameshambuliwa na mdudu huyu Kiwavijeshi mvaamizi amesema"Nilitembelea Shamba langu lenye ukubwa wa Hekari 2.5  nililolima zao la Mahindi na kuona majani yameshambuliwa kwa pembeni hivyo nikapiga dawa mara ya kwanza na yapili bila mafanikio hadi alipokuja Afisa kilimo siku ya Jana na kunielekeza vipimo sahihi ndipo wadudu hawa walikufa".

wakulima wameshukuru kupata elimu hiyo na kuahidi kuitumia pamoja na kuwafikishia wakulima wengine ambao hawakupata pia wameomba Serikali kuwapatia msaada wa  viuatilifu (dawa) za kumdibiti mdudu huyo  Kiwavijeshi mwaamizi hiyo kwa kudai kuwa viuatilifu hivyo  ni vya gharama .

Afisa Kilimo Eliudi Saoyo  akiwaelimisha wakulima wa Kijiji cha Nkoasenga juu ya mdudu mwaribifu mazao aitwae Kiwavijeshi kivaamizi (AMRY WORM)

Afisa Kilimo Eliudi Saoyo  akiwaonesha  wakulima wa Kijiji cha Nkoasenga mojawapo ya kiuatilifu cha kumdhibiti mdudu aitwaye Kiwavijeshi kivaamizi (AMRY WORM)

 wakulima wa Kijiji cha Nkoasenga  wakifuatilia semina ya mafunzo  juu ya mdudu mwaribifu mazao aitwae Kiwavijeshi kivaamizi (AMRY WORM) iliyotolewa na Afisa kilimo Eliud Saoyo.

 wakulima wa Kijiji cha Nkoasenga  wakifuatilia semina ya mafunzo  juu ya mdudu mwaribifu mazao aitwae Kiwavijeshi kivaamizi (AMRY WORM) iliyotolewa na Afisa kilimo Eliud Saoyo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nkoasenga Sifael K.Pallangyo  akieleza wakulima wenzake wa kijiji hicho namna alivyogundua uwepo wa mdudu Kiwavijeshi kivaamizi na kumdibiti.



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa