• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UJENZI NA UBORESHAJI WA KITUO CHA AFYA USA-RIVER NI MFANO WA KUIGWA.

Imewekwa: June 3rd, 2018

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege ameridhishwa na matumizi ya fedha kwenye ujenzi na uboreshaji wa Kituo cha Afya Usa- River  na kueleza kuwa  thamani ya fedha imeonekana pia ametoa  wito kwa Halmashauri nyingine kuiga mfano.

Mhe.Naibu Waziri Kandege amesema hayo alipokagua ujenzi na ukarabati wa kituo cha Afya Usa- River wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa vituo vya Afya vilivyopewa fedha na Serikali kwenye Mkoa wa Arusha kwaajili ya ujenzi wa majengo mapya na kukarabati yaliyopo kwa lengo la kutoa huduma bora za Afya,  pia Mhe.Naibu Waziri Kandege amemwagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Dkt. Cosmas Kilasara kutoa elimu ya kina kwa wananchi ili waweze kujiunga na mfuko wa Afya ya jamii CHF.

Aidha ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwenye  kituo hicho cha Afya Usa -River  ni baada ya Serikali kutoa fedha kiasi cha Sh. milioni 500 kwa ajili ya kuboresha kituo hicho kwa kujenga majengo  mapya ambayo ni jengo la maabara,nyumba ya mtumishi, jengo la upasuaji, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kuifadhia maiti, kichomea taka  pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yaliyokuwepo kwa lengo la kuwapa wananchi huduma bora za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. 

PICHA ZA TUKIO.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege(wakwanza kulia) akiwa na viongozi mbalimbali akiwemo  Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru, Ndg.Timotheo Mzava,Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Christopher Kazeri,Mganga mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Timoth Wonanji ,Mganga mkuu wa Halmashauri ya Meru Dkt. Cosmas Kilasara pamoja na wataalamu wenginewakitembelea na kukagua ujenzi kwenye kituo cha Afya Usa-River. 

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la Upasuaji kwenye kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la Upasuaji kwenye kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la kuwahudumia wagonjwa wa wa nje (OPD)

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la kuwahudumia wagonjwa wa wa nje (OPD)

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la wodi ya mama na mtoto kwenye kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea sehemu ya kufulia iliyopo kwenye wodi ya mama na mtoto kwenye kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea kichomea taka katika Kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akikagua  upauzi wa njia ya kuptia wagonjwa  .

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akitoa mrejesho wa ukaguzi wa  kituo cha Afya Usa-River.

Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher Kazeri .

                                                                             PICHA ZA MAJENGO.


Jengo la wodi ya Mama na Mtoto litapunguza vifovitokanavyo na uzazi pamoja na msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali yaWilaya.


Jengo la upasuaji pindi litakapoanza kutumika kwa kiasi kikubwa litapunguza vifovitokanavyo na uzazi pamoja na msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali yaWilaya.

 

Nyumba ya mtumishi itaboresha mazingira ya mtumishi kufanya kazi kwenye mazingira rafiki hivyo huduma za dharura kupatikana kwa urahisi.

Jengo la kuhifadhia maiti .        

Jengo la duka la dawa ambalo awali lilitumika kama kama jengo  la maabara.

Mwonekano wa ndani wa chumba cha upasuaji.

Mwonekano wa ndani kwenye jengo la wodi ya mama na mtoto.

Sehemuya kufulia kwenye Jengo la wodi ya Mama na Mtoto  ikiwa na uhakika waupatikanaji wa maji wakati wote kutokana na uwepo wa matanki ya kuifadhia maji.

Mwonekano wa ndani kwenye sehemu ya kufulia kwenye jengo la mama na mtoto.


Picha ya kichomea taka kipya kwenye kituo cha Afya  Usa-RIVER.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa