• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

"AFYA BORA NI HATUA YA KWANZA YA MAENDELEO"KAULI YA MKURUGENZI MERU KATIKA UZINDUZI WA MAFUNZO KWA MAAFISA WAANDIKISHAJI WA CHF ILIYOBORESHWA

Imewekwa: July 2nd, 2019

Mkurugenzi  mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Ndg.Emmanuel Mkongo, wakati akifungua mafunzo kwa waandikishaji wa mfuko wa bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa iCHF, ametoa wito kwa wananchi wa Halmashauri hiyo kujiunga na bima hiyo   ili wawe na uhakika wa huduma za Afya wakati wote .

Mkongo  amesema ni muhimu kwa jamii kulipa  suala la afya kipaumbele kwani ndio chanzo cha kwanza cha maendeleo ambapo amewataka waandikishaji hao kuzingatia mafunzo hayo kwa makini ili waweze kuifanya kazi hiyo ya uandikishaji kwa ufanisi, "bila nguvukazi ya kutosha inayotokana na afya njema hakuna maendeleo" amesisitiza Mkongo.

Mratibu wa CHF   Mkoa wa Arusha,Ndg.Erena Materu mbali na kuipongeza Halmashauri ya Meru  kwa kuharakakisha taratibu za uandikishaji wa bima hiyo ya CHF iliyoboreshwa ambapo ni Halmashauri ya pili katika Mkoa huo kutoa mafunzo kwa waandikishaji,ametoa wito kwa Mkuu wa idara ya Afya kuhakikisha pindi mwananchi anapojiunga na mfuko huo anapata huduma  kuanzia ngazi ya zahanati.


Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt.Maneno Focus amefafanua  kuwa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba  katika Halmashauri hiyo ni wa kuridhisha kwani asilimia 90 ya dawa muhimu zinapatikana na ameahidi kuendelea kusimamia vyema upaktikanaji wa huduma za afya kuanzia ngazi za Zahanati.

mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo toka Shirika la  Pharmaccess International linalofadhili mafunzo hayo,Ndg.Emmanuel Carl ameeleza kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau ilifanya utafiti wa changamoto za CHF ya zamani na kuzitafutia ufumbuzi kwa kuja na mfuko huu wa CHF iliyoboreshwa ambao utakaotoa huduma Nchi nzima .

Carl ameelezea kuna  manufaa makubwa kwa Kaya itakayojiunga na mfuko huu wa CHF iliyoboreshwa kwa kuchangia fedha  kiasi cha tsh.30.000 ,kwani Kaya hiyo itapata huduma za afya ikihusisha matibabu yote,vipimo ya maabara,uchunguzi kwa njia ya mionzi yaani X-ray na Ultrasound, huduma za afya ya kinywa na huduma za upasuaji zitatolewa katika mfuko huo kwa kufuata taratibu ambapo mwanachama ataanzia  Zahanati na kituo cha afya kilichopo karibu nae na ikibainika anahitaji matibabu ngazi nyingine atapewa rufaa  kwenda katika Hospitali ya Wilaya au Hospitali ya Rufaa ya Mkoa husika.

Carl  Amefafanua kuwa  bima ya  CHF iliyoboreshwa  haitohusika kupata huduma zote zinazohusisha madaktari bingwa wabobezi pamoja na vipimo vinavyotolewa na hospitali za rufaa za kitaifa za kanda .

kwa mujibu wa CHF iliyoboreshwa Kaya ni baba ,mama na watoto wanne wasiozidi umri wa miaka 18 pamoja na mwanakaya mwenye ulemavu ambaye imethibitika hana uwezo wa kujipatia kipato.Pia kwa wanafunzi wa wa Shule za Sekondari na vyuo vya mafunzo stadi taasisi zitahusika kuwaandikishwa wanafunzi wasiozidi 5 kwenye bima ya CHF Iliyoboreshwa.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa Siku mbili kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Meru yamejumuisha waandikishaji toka kata 26 za Halmashauri hiyo .

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru,Ndg.Emmanuel Mkongo.

Mratibu wa CHF   Mkoa wa Arusha,Ndg.Erena Materu

Mkuu wa Idara ya Afya Halmashauri ya Meru Dkt.Focus Maneno

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo toka Shirika la  Pharmaccess International linalofadhili mafunzo hayo,Ndg.Emmanuel Carl.

Mratibu wa CHF iliyoboreshwa wa Wilaya Tumaini  Mayeye

(Kushoto) ni Afisa Tehama Mkoa Obedi Mkuya na kulia kwake ni Steven Kauli Afisa Tehamaa Halmashauri ya Meru.

Maafisa Waandikishaji wa CHF iliyoboreshwa wakati wa mafunzo.

Maafisa Waandikishaji wa CHF iliyoboreshwa wakati wa mafunzo.



Maafisa Waandikishaji wa CHF iliyoboreshwa wakati wa mafunzo.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa