Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mhandisi Richard Ruyango ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Meru kudhibiti mimba za utotoni sambamba na utoro mashuleni.
Akizungumza Katika Baraza la Halmashauri hiyo, Ruyango ameagiza kuundwa kwa Kamati ya kuzuia na kupambana na mimba za utotoni ikiwa ni mkakati wa kumwezesha mtoto wa kike kufikia ndoto zake "tuwasaidie wafikie ndoto zao, kwani ni Madiwani, wakuu wa Wilaya na Viongozi wajao, mfano Mkurugenzi wa Halmashauri hii ni mwanamke "amehimiza Ruyango
Pia, Mhe. Ruyango ameielekeza kamati hiyo kuthibiti suala la utoro mashuleni ambapo amewataka wazazi wote ambao watoto wao ni watoro kufuatiliwa na kuchukuliwa hatua za kisheria pamoja na wazazi wote watakao husika kukwamisha udhibiti wa Mimba za utotoni kwa kuwaficha wenye hatia kuchukiwa hatua za kisheria.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango Akizungumza wakati wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Mhe.Jeremia Kishilu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru,wakati wa Mkutano wa baraza la Halmashauri
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya wakati wa Mkutano wa baraza la Madiwani.
Waheshimiwa Madiwani wakati wa Mkutano
Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Mkutano wa baraza la Madiwani.
Waheshimiwa Madiwani wakati wa Mkutano
Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Mkutano wa baraza la Madiwani.
Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Mkutano wa baraza la Madiwani.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa