• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANAFUNZI 96 KIDATO CHA KWANZA WAPANGWA AWAMU YA PILI

Imewekwa: January 26th, 2021

Wanafunzi  96  katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambao ni miongoni mwa wanafunzi 1,635 wa kidato cha kwanza  ambao hawakupangwa katika awamu ya kwanza kutokana na upungufu wa  vyumba vya madarasa,  wamepangwa katika Shule ya Sekondari Nkoarisambu baada  vyumba viwili kukamilika.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndg.Emmanuel Mkongo amesema  Halmashauri hiyo imeanza kuwapanga wanafunzi wa kidato  cha kwanza kwa awamu ya pili, ambapo leo  wanafunzi 96  wamepangwa katika  shule ya Sekondari Nkoarisambu hivyo kutimia kwa idadi ya wanafunzi 196 waliopangwa katika shule hiyo. Ameeleza kuwa kutokana na upungufu wa vyumba 2 vya madarasa wanafunzi 100 pekee  walipangwa katika shule hiyo  kwa awamu ya kwanza.

Mkongo amesema Halmashauri hiyo itaendelea kuwapanga wanafunzi wa awamu ya pili katika shule za Sekondari zitakazo kamilisha  vyumba vya madarasa  baada ya kufanya ukaguzi na kujiridhisha. Mkongo ameendelea kutoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani ,Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji, Watendaji wa Kata na Vijiji kusimamia ukamilishaji  wa madarasa hayo kabla ya tarehe 28 Febriari 2021 kama Serikali ilivyoelekeza.

Aidha, ziara hiyo ya Ufuatiliaji na Ukaguzi wa ukamilishaji  wa vyumba vya  madarasa ilimjumuisha Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Jeremia  Kishili, Mkurugenzi, Afisa elimu Sekondari na Mhandisi  wa ujenzi. Shule za Sekondari  zilizo tembelewa ni  Ngongongare,  Nkoarisambu na Shule mpya ya Sekondari Kiwawa inayotarajiwa kuanza wiki ijayo kwa kupangiwa wanafunzi ,  shule hii ni mpya ina vyumba vya 4 vya madarasa, viti na meza 100  kwaajili ya wanafunzi,  imeelekezwa kukamilisha  baadhi ya miundombinu ya maji kwa upande wa vyoo vya Ofisi ya Walimu kabla ya wiki ijayo.

Ikumbukwe, katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru idadi ya wanafunzi 6,851 walichaguliwa kujiunga kidato cha kwanza ambapo kati yao 5,216 walipangwa kwa awamu ya kwanza na 1,635 wanasubiri kupangwa kwa awamu ya pili baada ya vyumba vya madarasa kukamilika ambapo kati yao 96 wamepangwa leo.

Katika kuhakikisha vyumba vya madarasa vinakamilika Halmashauri ya Wilaya Meru kupitia fedha za mapato yake ya ndani (Own Source) imetumia zaidi ya Shilingi Milioni 160 kununua vifaa vya ujenzi ambavyo ni Bati 1860 zilizogharimu  shilingi 48,259,004.51, Mbao shilingi 64,598,752.00 na Saruji mifuko 3325 iliyogharimu  shilingi 48,212,500.

bofya hapa Kuona orodha ya wanafunzi 96 waliopangwa.pdf

Mkutugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ta Meru akiwa katika moja ya darasa katika Shule ya Sekondari Nkoarisambu.

Uongozi wakati wa Ziara katila shule ya Sekondari Kiwawa.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa