• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MIMBA ZA UTOTONI KUWA AGENDA YA KUDUMU MERU DC..

Imewekwa: November 8th, 2018

Wajumbe wa baraza la madiwani Halmashauri ya Meru, wilayani Arumeru, wamekubaliana kuwa na agenda ya kutokomeza mimba za utotoni na utoro shuleni kudumu kwenye vikao vya Vijiji na Kata kwa kujikita kuelimisha jamii kuanzia ngazi ya familia. 

Wajumbe hao wameazimia hilo, mara baada ya, madiwani wa Kata kadhaa kuwasilishwa taarifa zinazoonesha changamo ya mimba za utotoni zinazowaka bili wanafunzi katika kata zao. 

Awali taarifa hizo zimethibitishwa na Idara ya Elimu Msingi na Sekondari kuthibitisha kuwa jumla wanafunzi 67 wamepata mimba  kwa mwaka 2017/2018. 

Afisa elimu Sekondari Mwl Damari Mchome ameeleza  kuwa kwa kipindi cha Mwezi Jan uari 2017 mpaka sasa jumla ya wanafunzi 57 waliripotiwa kupata mimba ambapo kati yao  wanafunzi 27 wamepata mimba kuan zia mwezi Januari mwaka huu 2018.

Mwl.Mchome ametoa rai kwa wazazi kutekeleza jukumu la malezi kwa wanafunzi sambamba na kujenga mabweni ili kuwaepusha wanafunzi  hao wa kike  na vishawishi  wanavyokutana navyo kwa kutembea umbali mrefu kwenda shule .

Nae mwakilishi wa Afisa elimu Msingi Mwl.Exaud Kimaro ameeleza kuwa  kwa kipindi cha Mwezi Januari Mwaka 2017 hadi Mwezi Octoba mwaka huu jumla ya wanafunzi 10 wa shule za Msingi wamepata mimba na kushindwa kuendelea na Masomo.

Mwanasheria wa Halmashauri hiyo,wakili Magdalena John amesema Serikali iliweka sheria ili kumlinda Mwanafunzi kutokukosa fursa ya masomo  ila changamoto kubwa katika kushughulika na  kesi za mimba kwa wanafunzi ni utoaji wa ushahidi hivyo ametoa rai kwa wazazi na jamii kutoa ushahidi kwa wakati.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Nelson Mafie amesikitishwa  na wazazi kutokua mstari wa mbele kutoa taarifa za wanafunzi kupata mimba na kusubiri viongozi kuja kuzitafuta. "tumeona hivi karibuni Mkuu  wetu wa Wilaya Jerry Muro akipambana kutokomeza mimba kwa wanafunzi kwa kuwachukulia hatua wahusika , hivi wazazi na jamii tunakuwa tupo wapi ?' " Amehoji Mafie .

"Halmashauri imejipanga vipi kumaliza swala la mimba kwa wanafunzi ?"amehoji Diwani viti maalumu Kata ya Usa -River Meri Antony 

Akihitimisha mjadala huo mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Will Njau, ametoa rai kwa viongozi wa dini ,mila na siasa kutoa elimu huku muongozo wa baraza hilo agenda ya kutokomeza mimba za utotoni kwa wanafunzi na utoro kuwa ya kudumu katika vikao ngazi za vijiji na kata .

Aidha Mkutano wa Baraza la Halmashauri ya Meru kwa kipindi cha Robo  ya kwanza Julai -Septemba umekamilika kwa siku ya kwanza ambapo  madiwani 3   toka Kata ya Kikwe,King'ori na Majengo walioshinda uchaguzi mdogo uliofanyika tarebe 13 Mwezi  Octoba mwaka  huu wameapishwa

Katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Willy Njau ,kulia kwake ni Makamu Mwenyekiti Nelson Mafie na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Emmanuel Mkongo.

Mwakilishi wa Afisa elimu Msingi ,Mwl.Exaud Kimaro akitoa taarifa yawanafunzi wa shule za msingi waliopata mimba

Afisa elimu Sekondari,Mwl.Damari Mchome akitoa taarifa yawanafunzi wa shule za sekondari waliopata mimba.

Mwanasheria wa Halmashauri ya Meru ,wakili Magdalena John akitoa ushauri wa kisheria katika baraza la Halmashauri.

Mhe. Diwani Kata ya Imbaseni Gadiel Mwanda  akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe.Elisa Mungure Diwani Kata  ya Kikatiti  akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe. Peter Kessy Diwani Kata ya King'ori akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe.Anderson Sikawa  Diwani Kata ya Leguruki akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe.Bernad Kivondo Diwani Kata ya Majengo akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe. Diwani Kata ya Makiba Samson Laizer akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe.Diwani Kata ya Ngarenanyuki Zakaria Nnko akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Mhe.Charles NnkoDiwani Kata ya Songoro akiwasilisha taarifa ya kata hiyo katika baraza la Halmashauri.

Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Wakuu wa idara na vitengo wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.

Wakuu wa idara na vitengo na wananchi wakisikiliza taarifa za wanafunzi waliopata Mimba.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa