Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Wilayani Arumeru lapitia na kuridhia taarifa ya ufungaji wa hesabu za mwisho za mwaka wa fedha 2021/2022, ambapo limeazimia kuongeza mapato ikiwa ni pamoja na kubuni vyanzo vipya ili Halmashauri kuongeza uwezo wa kujiendesha na kuwaletea wananchi maendeleo .
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru Mhe.Jeremia Kishili amesema ukusanyaji wa mapato umekuwa ukiongezeka kutokana na mikakati iliyowekwa na madiwani kwa kushirikiana na wataalum inayolenga kuwaletea wananchi wa Meru Maendeleo.
Awali, Akiwasilisha taarifa ya ufungaji wa Hesabu za mwisho za mwaka wa fedha 2021/2022, Mweka hazina wa Halmashauri ya Meru Zubeda Nkuba amesema taarifa hiyo imeandaliwa kwa mujibu wa kifungu cha 6 (d) na 7 (d) cha Memoranda ya Fedha ya mwaka 2010 .
Baraza hilo maalumu la kupitia taarifa ya ufungaji wa hesabu za mwisho za mwaka wa fedha 2021/2022 limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri .
MERU TUPO VIZURI KAZI IENDELEE
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru Mhe.Jeremia Kishili wakati wa kikao.
Waheshimiwa Madiwani wakati wa kikao.
Waheshimiwa Madiwani wakati wa kikao
Waheshimiwa Madiwani wakati wa kikao
Waheshimiwa Madiwani wakati wa kikao
Wataalam wakati wa kikao
Waheshimiwa Madiwani wakati wa kikao
Baadhi ya Wataalum wakati wa kikao
Mweka hazina wa Halmashauri ya Meru Zubeda Nkuba
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa