• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Baraza la Madiwani lapitisha Bajeti,Shilingi bilioni 55.5

Imewekwa: February 11th, 2022

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Meru, lapitisha rasimu ya  Mpango wa Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha ujao 2022/2023, kiasi Cha Shilingi bilioni 55.5 ikiwa ni ongezeko la asilimia 8% ikilinganishwa na bajeti ya Mwaka wa fedha unaoendelea.

Akizungumza wakati wa mkutano huo,Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili,  amethibitisha baraza hilo kupitisha Mpango wa bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka ujao wa fedha kiasi cha shilingi bilioni 55.5 kwa mchanganuo wa ,mapato ya ndani Shilingi Bilioni 6.7, Ruzuku ya Mishaara ya Watumishi Shilingi Bilioni 36.18, Ruzuku ya kawaida Shilingi Bilioni 1.18 na miradi ya maendeleo Shilingi Bilioni 11.45.

Aidha Mhe.Kishili amemshukuru Rais.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa  fedha za maendeleo katika sekta ya Elimu, afya, Maji na  barabara katika Halmashauri ya Meru. Pia  amewapongeza wataalam wa Halmashauri hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi Zainabu kwa Kushirikiana vyema kuleta maendeleo katika Halmashauri hiyo sambamba na wadau mbalimbali wa maendeleo na kutoa wito ushirikiano huo kuwa endelevu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amesema ongezeko Hilo la asilimia 8% ya bajeti ya Mwaka 2022/2023  inatokana na uibuaji wa vyanzo vipya vya mapato na hali halosi ya makusanyo hadi Disemba 2021, ambapo ametoa mfano bajeti ya  mapato ya ndani yasiyofungiwa  yameongezeka kwa asilimia 44% kutoka Shilingi Bilioni 2.18 2021/2022 hadi Bilioni 3.1 Mwaka wa fedha  ujao  2022/2023

Mwl.Makwinya amesema, kipaumbele chake ni ukusanyaji wa mapato yatakayotumika kuwaletea Wananchi maendeleo ambapo katika mikakati ya kufanikisha hilo wameshakutana na wenyeviti wa Vijiji na watendaji wa Kata na wanataraji kukutana nao tena na Watendaji hao kwa pamoja na wenyeviti wa vijini na watendaji wa vijiji Ili kuhakikisha mapato yanakusanywa.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango ameipongeza Rasimu ya bajeti ya Halmashauri ya Meru kwa Mwaka 2022/2023 kwa kiasi kikubwa inakidhi hali halisi ya Halmashauri hiyo.  Pia amewakumbusha Waheshimiwa Madiwani kujiandaa na Swala la Sensa ya watu na Makazi linalotarajiwa kuanza mwezi Agasti 2022.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Waheshimiwa Madiwani  mbali na kuipongeza rasimu hiyo kuwa na tija kwa wanameru  wameonesha kuendelea kushirikiana kuwaletea Wananchi  wa Meru maendeleo  ambapo wameamua Shilingi Milioni 26 katika bajeti inayoendelea , zilizokuwa zimetengwa kama fedha za Utengenezaji wa miundombinu ya  barabara kila Kata kwa mgao wa Shilingi Milioni Moja kupeleka kuchimbua korongo la Mto nduruma ambalo  ni changamoto kubwa kwa Wananchi wa Kata ya Shambarai Burka , Maroroni na Mbuguni.

"Tunashukuru sana Baraza la Madiwani kuafiki fedha Milioni 26 kutatua  changamoto hii ya korongo la mto Nduruma kwani wakati wa Mvua barabara zinajaa Maji Kinamama  wanapata sana tabu na wanafunzi pia" Mollel Diwani wa Kata ya Shambarai Burka .


Ikumbukwe

Mpango huo wa bajeti umeandaliwa kwa mujibu wa kifungu Na. 11 cha  sheria ya Sheria ya Bajeti Na. 21 ya mwaka 2015 pamoja na Kanuni zake, maelekezo na mwongozo wa kitaifa maandalizi ya Bajeti, unaoelekeza  kupokea mapendekezo na vipaumbele kisekta kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji, kata, Idara na Vitengo vya halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa