• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MKUU WA MKOA WA ARUSHA ARIDHISHWA NA UJENZI NA UKAMILISHAJI WA VYUMBA VYA MADARASA MERU

Imewekwa: January 7th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Idd Kimanta,amepongeza juhudi za   ukamilishaji wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru Wilayani Arumeru.

Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya siku mbili katika Wilaya ya Arumeru ambapo kwa siku ya kwanza imeanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru na siku ya pili itakuwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.

Akisoma taarifa mbele ya Mkuu huyo wa Mkoa, Mkuu wa Shule ya Sekondari Patandi Maalum Mwl.Janeth Mollel amesema mbali na Serikali kutumia zaidi ya Bilioni 3.4 kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule hiyo ya mfano nchini bado kunauhitaji wa ukamilishaji wa miundombinu muhimu na rafiki yenye thamani ya shilingi milioni 800 ili kuwezesha kuwapokea wanafunzi 185 wa kidato cha kwanza waliopangwa shuleni hapo.

Mwl.Molel amechanganua kuwa kati ya Wanafunzi 185  wanafunzi 136 ambapo wavulana ni 66 na wasichana ni 70 ni wanafunzi wenye mahitaji maalum wa bweni  nMheshimiwa Idd Kimanta,na wanafunzi 49 waliobaki ni  wa kutwa.

Mwl. Mollel amesema miundombinu iliyokamilika  shuleni hapo ni mabweni manne ,mawili ya wasichana na mawili ya wavulana , madarasa 12 ya kidato cha kwanza hadi kidato cha nne, kwa utaratibu wa madarasa 3 kwa kila kidato kwa wastani wa wanafunzi 47.
 
Aidha. Mwl. Mollel amesisitiza kuwa kwa kuzingatia wanafunzi 136 waliopangwa ni wenye mahitaji maalumu kuna haja ya kutatua  changamoto ya   mahitaji muhimu ambayo mi vitanda double deka 10, magodoro 20, viti na meza 80 kwaajili ya matumizi ya wanafunzi darasani pamoja na ujenzi wa maabara ya sayansi, kuongeza mfumo wa maji taka, kuchimba kisima cha maji na mfumo wa kusambaza maji, kujenga mfumo wa jiko la gesi na jiko la tahadhari la kuni na ujenzi wa nyumba tatu kwa ajili ya Mwalimu, Patroni na Matroni pamoja na kuajiri Watumishi muhimu kwa Wanafunzi wenye mahitaji maalum.  

Naye Ndg.Emmanuel Mkongo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya MERU amesema katika kutatua changamoto hizo Halmashauri hiyo imefanya juhudi za kuomba fedha za mahitaji muhimu katika Ofisi ya Rais TAMISEMI.  Aidha, kutokana na changamoto za ukosefu wa miundombinu hiyo na kusubiri kupokelewa kwa fedha za ujenzi, Halmashauri imeandika barua Ofisi ya Rais TAMISEMI kuomba muongozo wa kusogeza muda wa kuwapokea wanafunzi hao kwa miezi mitatu (3) ili kukamilisha miundombinu hiyo ikiwemo uchimbaji wa kisima na miundombinu ya maji safi na salama, mfumoza wa maji taka ,
jenereta,ujenzi wa kuchomea taka,nyumba za kuishi mwalimu mkuu sambamba na mahitaji ya rasilimali watu, "wanafunzi hawa wenye uhitaji maalumu  wanahitaji mazingira bora na wezeshi "amesisitiza Mkongo.

 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndg.Jerry Muro amesema  Serikali imewekeza sana katika shule hiyo lakini hadi sasa bado wanasubiri mwongozo kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI kwani  fedha zaidi ya shilingi milioni 800  zinahitajika kukamilisha miundombini rafiki kwa wanafunzi shuleni hapo.

Akihitimisha ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru , Mkuu wa Mkoa wa Arusha  amesitisha kuanza rasmi kwa shule hiyo tarehe 11 mwezi huu na kuahidi kutafuta ufumbuzi mapema ili  wanafunzi hao waweze kuanza masomo yao.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua Vyumba vya Madarasa katika Shule za Sekondari za Akheri, Patandi Maalum, Nshupu, Sing'si, Kikwe na  Muungano pamoja na Shule mpya ya Msingi ya Faye Crene Chem Chem iliyojengwa kwa ufadhili wa  Rotary Club.
 



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa