• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MERU,MWITIKIO MKUBWA CHANJO YA UVIKO -19

Imewekwa: August 3rd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Eng.Richard Ruyango ametoa wito kwa Viongozi wa jamii, madhehebu ya dini  kuelimisha Umma juu ya huduma za chanjo ya UVIKO - 19 ikiwa fursa kwa wananchi ambao wapo tayari kuchanjwa na kupunguza athari za kupata ugonjwa na madhara makubwa.

Eng.Ruyango ametoa Wito huo wakati wa  uzinduzi wa chanjo ya UVIKO - 19  katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambao umefanyika katika Kituo cha Afya chw Usa-River .

Aidha,Ruyango amewataka Wananchi kuchukua tahadhari ya ugonjwa huu ambapo amepiga marufuku mikusanyiko kwenye misiba pia ametoa wito kwa Viongozi wa Dini kufupisha Ibada  na kuwakumbusha waumini kuchukua tahadhari.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt.Maneno Focus amesema chanjo ya UVIKO -19 ni afua nyingine katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19 ambapo walengwa 5410 wanatarajiwa kupata chanjo katika awamu ya kwanza ambapo ameanisha makundi yatakayoanza kupata chanjo ni pamoja na watumishi wa afya,walimu,vyombo vya ulinzi na usalama ,wenye magonjwa Sugu na wazee.

Nao Wanachi ambao wamepata fursa ya kupata chanjo ya UVIKO - 19 wameishukuru Serikali kwa kuleta chanjo hiyo na kuiomba mbali na kuchanjwa makundi yaliyoainishwa iendelee kupanua wigo wa utoaji chanjo hiyo kwa makundi mengine.

Aidha, Katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mheshimiwa Eng.Richard Ruyango amekuwa wa kwanza kupata chanjo hiyo akifuatiwa na Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel John Mkongo ambaye amehamishiwa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, Viongozi wa Dini akiwemo Askofu Mkuu wa Kanisa  la KKKT Dayosisi ya Meru, Paroko wa Parokia ya USA RIVER, Viongozi wa vyama vya Siasa ,Waheshimiwa Madiwani na wawakilishi wa watu wenye ulemavu.

Zoezi hilo linatarajiwa kuendelea katika vituo vya Hospitali ya Wilaya ya Meru na Kituo cha Afya Usa River.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Eng.Richard Ruyango wakati wa chanjo ya UVIKO - 19

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Eng.Richard Ruyango akichanjwa chanjo ya UVIKO - 19.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Eng.Richard Ruyango akiwa na Cheti baada ya  kuchanjwa chanjo ya UVIKO - 19.


Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt.Maneno Focus akichanjwa chanjo ya UVIKO - 19

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel John Mkongo akipigwa chanjo ya UVIKO -19

mwenyekiti wa kamati ya Elimu afya na maji Halmashauri ya Meru,Diwani wa Kata ya Songoro akipata chanjo ya UVIKO-19

Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Arumeru Ngd.Deo Mtui akipata Chanjo ya UVIKO -19.

Askofu wa KKKT Dayosisi ya Meru Elias Kitoi Nassari wakati wa Chanjo ya UVIKO -19.

Askofu wa KKKT Dayosisi ya Meru Elias Kitoi Nassari wakati wa Chanjo ya UVIKO -19

Askofu  Issangya wa Sakila International Evangilism akiwa na Cheri baada ya kupata chanjo ya UVIKO -19.

Mhe.Diwani wa Kata ya USA - River baada ya kupata chanjo ya UVIKO -19




Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa