Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango amezindua rasmi kampeni ya awamu ya tatu ya chanjo ya Polio itakayofanyika kwa Siku nne kuanzia leo tarehe 01 hadi 4 Septemba 2022, ambapo ametoa wito kwa jamii kuwalinda watoto dhidi ya ugonjwa Polio unaosababisha kupooza na ulemavu wa viungo, kwa kuhakikisha watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano wanapata chanjo.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika hospitali ya Wilaya ya Meru (tengeru) Mhe. Ruyango amesema baada ya kugundulika uwepo wa ugonjwa huo nchi ya jirani ya Malawi Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan imehakikisha chanjo zinapatikana na watoto wanakuwa salama" chanjo ya Polio ni bure ni wasihi tuwalinde watoto kwa kuwapa chanjo"amehimiza Mhe.Ruyango
Dkt.Focus Maneno ambaye ni Mkuu wa Idara ya huduma za Afya, Lishe na ustawi wa jamii amesema ugonjwa wa polio hauna tiba na ni hatari kwani unasababisha mtoto kupooza hivyo kupata ulemavu wa viungo na kusababisha mtoto kuwa tegemezi ambapo amehimiza wazazi na walezi kuzuia madhara ya Polio kwa kuhakikisha watoto wanapata chanjo " mtoto asiyepata chanjo ni hatari kwake na kwa jamii nzima" amehimiza Dkt.Maneno.
Naye Mratibu wa chanjo Halmashauri ya Wilaya ya Meru Salome Mbegela amesema chanjo ya polio itatolewa kwa siku nne kuanzia leo tarehe 1 hadi 4 Septemba 2022 na itatolewa nyumba kwa nyumba, vituo vya huduma za afya, vituo vya kulelea watoto, katika shule nk
Bryson Willium ambaye ni mzazi mwenye mtoto aliyepata chanjo ametoa wito kwa wazazi wote kushiriki kuwapa watoto chanjo ya Polio kwani ugonjwa huo ni hatari " nitoe wito kwa kina baba wote kuwa mstari wa mbele kuwasaidia watoto kupata chanjo ya Polio kwani ni wajibu wa kila mzazi (baba na mama )na jamii yote kuwalinda watoto dhidi ya magonjwa ikiwa ni pamoja na Polio" amesema Bryason
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili ametoa wito kwa jamii kushiriki zoezi la chanjo ya Polio kuzuia ulemavu wa viungo unaosababisha kupooza kutokana na ugonjwa wa polio
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwiya ametoa wito kwa jamii kuhimizana ili watoto wote wenye umri chini ya miaka 5 wapate chanjo hiyo.
Ikumbukwe Halmashauri ya Wilaya ya Meru inatarajia kutoa chanjo ya Matone ya Polio kwa watoto elfu 56,591
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa