• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

CTSI YATOA MSAADA SEKONDARI YA KING'ORI BAADA YA KUUNGULIWA NA BWENI

Imewekwa: July 1st, 2024

Shirika lisilo la kiserikali la "Cross Talent Share International"(CTSI) limetoa msaada wa vitu vyenye thamani ya sh.Mil 5.5 katika shule ya Sekondari King'ori baada ya kupata majanga ya kuunguliwa na Bweni la wasichana.

Mwakilishi wa shirika la CTSI Bw. Justin Mwaisemba amekabidhi msaada huo shuleni hapo leo ikiwa ni pamoja na Magodoro 66, Mashuka 150 pamoja na vyandarua 66 kama sehemu ya kuwaandalia mazingira mazuri ya kusoma kwa kipindi ambacho shule zimefunguliwa.

"Mkurugenzi wa CTSI Bw. Hyeonseok Kim amewapa pole sana na ametamani sana angeshiriki katika zoezi hili lakini amepata dharura na majukumu nchini Korea na kunituma nimwakilishe ili kukabidhi msaada huu. Amesema Mwaisemba .

Aidha, ameeleza kuwa wao kama shirika wanaendelea kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Meru na kwa sasa wanajiandaa kwa ajili ya kusaidia kukarabati bweni lililoungua.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Meru Mwl. Zainabu J. Makwinya ametoa shukrani kwa shirika hilo ambalo limekuwa likitoa ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Meru.

" Natoa shukrani kwa Shirika la CTSI kwa kutusaidia kurudisha furaha kwa wanafunzi hawa kwani mara tulipopata tatizo walikuwa tayari na waliahidi kutoa msaada huo shule itakapofunguliwa.

Ameeleza kuwa CTSI wamekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwani wamechangia miradi ya maendeleo mingi katika Halmashauri ya Meru kama vile Ujenzi wa Madarasa, Vituo vya Afya na Zahanati.

Diwani Kata ya Malula Mhe. Lukumbwe Ndossi ameeleza kuwa chanzo cha Moto bado hakijafahamika lakini wameanza kuchukua tahadhali ya majanga ili yasitokee  tena. Pia, ametoa shukrani kwa Mfadhili huyo kwani kitendo hicho kitawasaidia wanafunzi kupata utulivu katika masomo.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa