• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC ARUMERU AAGIZA BILIONI 1.057 ZA MIRADI YA MAENDELEO KUTUMIKA KWA UADILIFU, UAMINIFU MKUBWA

Imewekwa: October 10th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango amewataka wakuu wa shule, watendaji wa Kata na Maafisa Elimu Kata na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuhakikisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo kiasi cha Bilioni1.057 zilizogawiwa kwenye maeneo yao kuhakikisha zinatumika kwa uadilifu  na uaminifu mkubwa ili kufikia azma ya Serikali ya kuboresha sekta ya elimu na afya na kuharakisha  Maendeleo nchini.


Mhandisi Ruyango amesema hayo wakati wa kikao na Wakuu wa Idara na Vitengo , Wakuu wa Shule zilizopelekewa fedha , Watendaji wa Kata na Maafisa Elimu Kata  kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri  hiyo, ambapo amehimiza fedha hizo za miradi kutumika kama Serikali ilivyokusudia. " Tunamshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutuletea fedha Bilioni 1.057 za miradi , niwatake muwe waadilifu, waaminifu na wazalendo katika kutekeleza miradi hii na ikakamilike kwa wakati" amehimiza Ruyango

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amesema Halmashauri hiyo imenufaika kuletewa Bilioni 1.057 za ujenzi wa vyumba 17  katika shule 14  za Sekondari,ujenzi wa vyumba 9  vya madarasa katika  shule 3 za msingi, ukamilishaji vyumba 6 vya madarasa katika shule sita za msingi, ujenzi wa nyumba nne  za walimu (two in one)  katika shule 4, ujenzi wa uzio wa shule ya msingi patandi ,ukamilishaji  wa mabweni 4 katika shule nne  za Sekondari, ujenzi wa bwalo moja  na ukamilishaji wa nyumba moja ya mtumishi wa afya.

Naye, Mhe.Jeremia Kishili, mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya  Meru kwa  niaba ya wananchi wa Halmashauri hiyo , ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha za miradi katika Halmashauri na kuhimiza wataalamu kutoa ushirikiano kwa wakati ili miradi ikamilike kwa wakati ambapo amehimiza ushirikiano baina na viongozi.

Kikao hicho cha uelewa wa pamoja kimefanyika katika  ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambapo kimejumuisha Uongozi wa Halmashauri,Kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya ya Arumeru,Wakuu wa Idara na Vitengo ,Watendaji wa Kata ,Wakuu wa Shule na Walimu wakuu wa shule  zenye Miradi  ambapo msisitizo umewekwa wa ukamilishaji miradi kwa wakati, uadilifu,weledi na  uzalendo na uaminifu mkubwa  katika kutekeleza miradi hiyo ya maendeleo.

Ikumbukwe katika fedha hizo zote kiasi cha shilingi Milioni 120 ni fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ,Meru Kazi iendelee

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango akizungumza wakati wa kikao.

Mhe.Jeremia Kishili, mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya  Meru akizungumza wakati wa kikao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya akizungumza wakati wa kikao.

Wakuu wa Shule na Walimu wakuu wa  zilizopelekewa fedha ,Watendaji wa Kata na Maafisa Elimu Kata wakato wa kikao.

Wakuu wa Idara na vitengo na wataalam wa sekta za ujenzi ,elimu nk wakati wa kikao

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa