• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC ARUMERU ATOA SIKU 14 KWA VIONGOZI KIJIJI CHA KISIMIRI JUU NA LOSINONI KUWASILISHA MAPENDEKEZO UTATUZI MGOGORO WA ENEO LA MALISHO LEKISHORI

Imewekwa: October 4th, 2021

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, ametoa siku 14 viongozi wa vijiji vya Kisimiri Juu, kata la Uwiro Halmashauri ya  Wilaya ya Meru na kijiji cha Losinoni Kata ya Oldonyowasi, Halmashauri ya Arusha, kukaa vikao na kutoa mapendekezo ya maridhianao lengo likiwa kutatua mgogoro wa eneo la malisho katika Mlima Lekishori, eneo linalogombewa na  wananchi wa pande hizo mbili.


Mhe.Ruyango ametoa agizo hilo baada ya kukutana na wananchi wa vijiji hivyo viwili kwa nyakati tofauti ambapo  kila upande umeonyesha hauna shida na upande mwingine, lakini kila upande ukilalamikia upande mwingine kuwa, ndio chanzo cha mgogoro huo unaohusisha eneo  hilo la malisho, linalodaiwa kutengwa miaka mingi iliyopita na wazee wao, kwa ajili ya malisho ya mifugo"Nawatoa siku 14, nendeni mkakae kila kila Kijiji na viongozi wake, mkalete mapendekezo ya maridhiano ya nini kifanyike ili kumaliza mgogoro huo, makubaliano  hayo yawasilishwe ndani ya siku hizoo 14,  kwaajili ya utekelezaji, lengo letu kubwa ni kumaliza mgogoro huu, ili wananchi  waendelee kuishi kwa amani na utulivu,ameagiza Ruyango

Viongozi hao wa Vijiji  wameweka wazi kuchoshwa na mgogoro huo ambao unawaumiza  wananchi wa pande zote mbili kwani unarudisha nyuma maendeleo katika maeneo yao, kutokana na wananchi kutumia muda mwingi kwenye malumbano, badala ya kujikita kwenye shughuli  za maendeo, pia  umesababisha  watu kupoteza  mali zao,unahatarisha Maisha nk.

Katika mikutano hiyo, mkuu wa wilaya ya Arumeru aliambatana na mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Salekwa, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, mkurugenzi mtendaji halmshauri ya Meru, Mwl.Zainabu Makwinya pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Arumeru.

Viongozi watakao husika kuandaa mapendekezo hayo ni pamoja na wawakilishi wa  wananchi wakiwemo wenyeviti wa vijiji vya Losinoni Juu na Kisimiri Juu, Waheshimiwa  Madiwani wa kata hizo mbili za Uwiro na Oldonyowasi, Maafisa watedaji wa vijiji na Kata zote mbili, Maafisa Tarafa wa Tarafa hizo mbili pamoja na viongozi wa mila.

BAADHI YA PICHA ZA TUKIO.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisimiri Juu kata ya Uwiro, Halmashauri ya  Wilaya ya Meru

Wananchi wa kijiji cha  Losinoni Juu kata ya Oldonyowas wakati wa mkutano wa hadhara uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru,

Mwananchi wa kijiji cha  Kisimiri Juu kata ya Uwiro, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, akizungumza na viongozi wa mila 'Malaigwanani' wa vijiji vya Kisimiri Juu na Losinoni .


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa