• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC KAGANDA ATOA MAELEKEZO KWA WASIMAMIZI WA VYOMBO VYA WATOA HUDUMA YA MAJI NGAZI YA JAMII

Imewekwa: November 1st, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda ametoa maagizo kwa wasimamizi wa Vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya Jamii kuhakikisha wanakuwa waaminifu katika ukusanyaji wa Fedha za miradi ya maji na kufanya kazi kwa bidii.

Mkuu wa Wilaya hiyo ametoa maelekezo katika Mkutano Mkuu wa nusu mwaka kwa Vyombo vya watoa huduma ya Maji ngazi ya Jamii (CBWSOs) ( BI - ANNUAL COMMUNITY OF PRACTICE MEETING) RUWASA Wilaya ya Arumeru uliofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii kilichopo Tengeru.

"Ninawaagiza kufanya kazi kwa bidii na kuwa waaminifu katika ukusanyaji wa fedha za miradi ya maji pamoja na usimamizi wa ukarabati mkubwa na mdogo katika miradi hiyo. Aidha, hatua zitachukuliwa kwa wale wote watakaokiuka na kuvunja taratibu. Hili ni pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wananchi wanaoharibu vyanzo vya maji" Alisema Kaganda.

Vilevile Mhe. Kaganda ameeleza kuwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 imezingatia na imeelezea umuhimu wa maji ambapo Sura ya 3 Ibara ya 97 ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi imeeleza kuwa maji ni msingi wa uhai wa binadamu na injini ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii hivyo upatikanaji wa uhakika wa huduma ya maji safi na salama na usafi wa mazingira huchangia sana katika kuzuia magonjwa na hivyo kuimarisha afya na kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla.

Meneja RUWASA Mkoa Wa Arusha Eng. Joseph Makaidi ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maji kwa Wilaya ya Arumeru. Pia amemshukuru Mhe. Kaganda kwa ufuatiliaji na utatuzi wa changamoto za miradi ya maji.

Hata hivyo Meneja Wa RUWASA Arumeru Eng. Shabib Wazir amewasilisha changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni pamoja na baadhi ya Taasisi kutolipa bili za maji, wananchi kukataa kufungiwa mita za maji na Serikali kutoshirikishwa katika miradi ya ufadhili ili iweze kusimamiwa na Serikali.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa