• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC MKALIPA AFUNGUA MAFUNZO YA UHAKIKI WA TAARIFA ZA ANWANI ZA MAKAZI MERU DC.

Imewekwa: February 1st, 2025

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari leo tarehe 7 Januari, 2025 wametoa mafunzo ya uhakiki wa taarifa za Anwani za Makazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Elimu Maalum Patandi - Tengeru.

Katika Ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Amir Mkalipa ambaye pia ni mgeni rasmi katika Ufunguzi wa mafunzo hayo, amewataka Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kuhakikisha baada ya mafunzo hayo waende kuhamasisha wananchi katika maeneo yao kushiriki kikamilifu katika zoezi la kuhakiki anwani za makazi.

"Niwaombe Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kutoa ushirikiano mkubwa katika zoezi hili kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata na Vijiji ili Wananchi wetu wafahamu kuwa hii ni fursa kwao kuhakiki taarifa zao lakini pia itarahisisha kuyatambua maeneo yetu kirahisi tofauti na njia zilizotumika awali." Amesema Mkalipa.

Aidha, Mhe. Mkalipa amewataka Wenyeviti hao kutoa taarifa kwa kamati ya Usalama ya Wilaya endapo kama watatokea watu watakaotaka kukwamisha zoezi hilo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Vilevile, Mkuu huyo amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru kusimamia zoezi hilo kikamilifu kwa kushirikiana na TARURA na TANROADS kuhakikisha Barabara zote zinakuwa na nguzo za majina ya Barabara.

Washiriki katika Mafunzo hayo ni Wakuu wa Taasisi wakiwemo TANROADS na TARURA, Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji pamoja na Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambao ndio walioendesha mafunzo hayo.Fungua Hapa Kutazama Video




Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa