• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WADAU WA ELIMU WATAKIWA KUTOA ELIMU INAYOJIKITA KWENYE SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

Imewekwa: October 2nd, 2019

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Ndg.Emmanuel Mkongo ametoa wito kwa wadau wanaotoa huduma ya elimu kutoa Elimu itakayoletatija kuelekea uchumi wa Kati .

Mkongo  amesema hayo wakati wa maafali ya 18  ya wanafunzi wanaotarajia kuhitimu kidato cha nne mwaka huu katika Shule ya Sekondari ya kisabato Tanzania TASS  inayomilikiwa na dhehebu la Kisabato  iliyopo katika Halmashauri ya Meru .

Aidha, Mkongo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafali hayo,amesema Serikali ya Awamu ya tano imeweka mipango ya kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025 kupitia uchumi wa viwanda unaotegemea Sayansi na Teknologia ,hivyo katika kutekeleza Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM ,ibara ya 52 inayoelekeza Serikali kuboresha Elimu, Serikali  inahakikisha watoto wa kitanzania wanapata elimu kuanzia ngazi ya awali mpaka elimu ya juu ambapo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali imetenga bilioni 288.5 kwaajili ya elimu bila malipo kwa shule za msingi na Sekondari,uboreshaji wa sekta ya Elimu umeongeza kwa kiasi kikubwa cha ufaulu ambapo Shule ya Sekondari ya Kata Kisimiri iliyopo katika Halmashauri hiyo imeongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2019.'Haya ni mafaniko makubwa ya Serikali ya awamu ya Tano kwa Shule ya Kisimiri ambayo ni ya Kata kufanya vizuri kuliko shule kongwe na za binafsi Nchini"amesisitiza Mkongo.


Aidha Mkongo amewasisitiza wahitimu hao kusoma kwa bidii na waweze kupata sifa ya kuchaguliwa kwa masomo ya Fizikia, Kemia, Hesabu na masomo ya sanaa,   kujiunga kidato cha tano katika Shule  hiyo Kinara Nchini, kwani Serikali huchagua wanafunzi kujiunga na shule zake bila ubaguzi  kwa lengo la kujenga taifa moja na kudumisha umoja na mshikamano .

Mkongo amesema uboreshaji wa Elimu unaenda sambamba hadi ngazi ya elimu ya juu ambapo Serikali hutoa mkopo kwa wanafunzi wanaokidhi vigezo waliosoma katika  Shule ya Serikali au Binafsi ,ambapo kwa mwaka huu  wa fedha 2019/2020 Serikali imetenga Shilingi Bilioni 450  kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi watakaojiunga na  Elimu ya juu watakaokidhi vigezo.

Mkongo amesisitiza kuna haja ya wadau wanao toa huduma ya elimu kuongeza juhudi ya kutoa elimu inayojikita katika Sayansi na teknolojia ili kuandaa nguvu kazi yenye ujuzi mahususi kwaajili ya uchumi wa viwanda kwakuwa kuna  uhitaji mkubwa wa vijana wabunifu na wajuzi katika kuelekea uchumi wa kati.

 Akihitimisha Mkongo amewaasa wahitimu hao 29, kufanya maandalizi kwa muda uliobakia ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wa kuhitimu kidato cha nne utakaofanyika kuanzia tarehe 04 hadi 22 Novemba 2019,pia amewataka wanafunzi wote kuwa na nidhamu na uadilifu ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao .

Mkuu wa Shule hiyo  Ndg. Borega Petro akisoma taarifa ya shule hiyo ameeleza kuwa shule hiyo mbali na kutoa Elimu imekuwa ikiwandaa kiroho na kiakili wanafunzi wake kuwa Raia mwema na watakao kuwa waadilifu na wazalendo..

Maafali hayo yamefanyika katika viwanja vya shule Hiyo iliyopo Kata ya Ngongongare karibu na Chuo kikuu cha ARUSHA,

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ,Ndg.Emmanuel Mkongo akizungumza wakati wa maafali Shule ya Sekondari TASS

Mkuu wa Shule ya TASS  Ndg. Borega Petro akisoma taarifa ya shule hiyo.

Wahitimu wakisoma Risala 

Wahitimu wakati wa Maafali.
Mgeni Rasmi ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru akikabidhi cheti kwa mhitimu .


Wazazi na walezi wakati wa maafali katika Shule ya TASS.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa