Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya ameagiza kasi ya ujenzi wa vyumba 70 vya Madarasa ya Uviko-19 kwenda sambamba na utengenezaji wa viti na meza.
Mwl.Makwinya ametoa agizo hilo wakati wa ziara ya ufuatiliaji wa ujenzi wa vyumba vya Madarasa hayo ambapo ametembelea ujenzi wa vyumba vya Madarasa katika shule nane(8) za Sekondari na kubaini nguvu kubwa kuwekezwa kwenye ujenzi wa Madarasa pekee "niwaelekeze Wakuu wa Shule, timu za ufuatiliaji na walezi wa Kata kuhakikisha ujenzi wa Madarasa unakwenda sambamba na utengenezaji wa viti na meza" ameagiza Makwinya
Vilevile Mwl.Makwinya amesema Miradi mingi imefikia hatua ya ufungaji wa lenta na upauzi, hivyo ameelekeza kwa miradi ambayo kasi yake ni ndogo Wakuu wa Shule kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kasi zaidi ikiwa ni pamoja na fundi kuwa na vibarua wa kutosha.
Aidha katika Ziara hiyo Mkurugenzi.Zainabu amekagua ujenzi wa Vyumba vya Madarasa katika shule za Sekondari, Momela, Umoja King'ori, Miririnyi, King'ori, Maruvango, Nkoasenga ,Nasholi pamoja na ujenzi wa Zahanati ya Mareu na bweni katika Shule ya Sekondari Nkoasenga .
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru (kilemba kichwani) wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa Shule ya Sekondari Momela,mradi unaogha rimu Tsh.Milioni 40, fedha za UVIKO -19
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa ukaguzi wa ukamilisha wa maboma ya madarasa(2) Shule ya Sekondari Umoja King'ori,mradi unaogharimu Tsh.Milioni 50, fedha za Tozo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa Shule ya Sekondari Miririnyi,mradi unaogharimu Tsh.Milioni 40, fedha za UVIKO -19
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa Shule ya Sekondari King'ori,mradi unaogharimu Tsh.Milioni 40, fedha za UVIKO -19
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Chumba kimoja (1) Cha darasa Shule ya Sekondari Nkoasenga,mradi unaogharimu Tsh.Milioni 20, fedha za UVIKO -19
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Bweni la Wanafunzi wa kike katika Shule ya Sekondari Nkoasenga, Ikiwa ni mchango wa wadau kuunga mkono uboreshaji wa miundombinu ya sekta ya elimu unaofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa Zahanati ya Mareu unaogharimu Milioni 250 fedha za tozo.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa