Msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, Ndg.Emmanuel Mkongo amemtangaza rasmi John D. Pallangyo wa chama cha Mapinduzi(CCM) kuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki na kumkabidhi cheti cha ushindi.
Aidha Mkongo Amesema kwa mujibu wa kifungu namba 66 (2 )cha sheria ya uchaguzi wa Rais na Wabunge ya mwaka 2015 na kifungu namba 81(b) cha sheria ya Taifa ya uchaguzi sura namba 345 mshindi wa uchaguzi hukabidhiwa cheti siku ya uchaguzi.
Aidha Mkongo amefafanua kuwa Kwa mujibu wa kifungu namba 45(2 )cha sheria za uchaguzi wa serikali za Mitaa,namba 4 ya mwaka 1979 sura 292. John D.Pallangyo alipita bila kupingwa kati ya wagombea 11 baada ya zoeli la uchukuaaji na urejeshaji fomu lililomalizika tarehe 19 Aprili 2019.
Mbunge John D. Pallangyo anatarajiwa kuapishwa na Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania hivi karibuni.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa