Tarehe 12 Disemba 2017,Halmashauri ya Meru imepokea jumla ya madawati 280 toka kwa Wakala wa Misutu shamba la Miti Meru/Usa kwaajili ya wanafunzi katika shule zake za Msingi tano ambazo ni Shule ya Msingi Kiwawa ambayo imepewa madawati 56, Shule ya Msingi Urisho imepewa madawati 56, Shule ya Msingi Sangananu imepewa madawati 56, Shule ya Msingi Ngongongare imepewa madawati 56 na Shule ya Msingi Sakila imepewa madawati 56.
Aidha Meneja wa Wakala wa msitu shamba la Meru/Usa Robert Faustine ameeleza kuwa wamefikia uamuzi huo wa kutengeneza na kukabidhi Wilaya ya Arumeru madawati 740 kwaajili ya Halmashauri zake mbili Meru na Arusha vijijini kwa ajili ya Shule zilizopo kwenye Vijiji vinavyopakana na shamba hilo kama tendo la kuiunga mkono Serikali ya awamu ya tano kwenye jitihada katika maswala ya maendeleo kwenye Sekta mabalimbali ikiwemo elimu kwa kuwezesha mazingira rafiki kwa Wanafunzi pia amefafunua kua ni utekelezaji wa ombi la aliyekua mkuu wa wilaya hiyo Mhe.Alexander P. Myeti ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Kaimu mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Idd H. Kimanta ,ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Monduli ameushukuru uongozi wa Shamba la Miti Meru/Usa kwa kuunga mkono Serikali ya awamu ya tano kwenye jitihada zake za kuboresha mazingira ya elimu na kuwezesha upatikanaji wa elimu bora kwa kila mtoto ,pia amewaagiza Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha Misitu iliyopo kwenye maeneo yao inahifadhiwa na kulindwa ili jamii inufaike na faida za Misitu hiyo.
Walimu wakuu wa shule zilizonufaika na mgao huu wa madawati wameushukuru uongozi wa shamba hilo la miti na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuchangia shughuli za maendeleo kwenye jami.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa