• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU YAKABIDHI MILIONI 93 KWA VIKUNDI 33

Imewekwa: October 12th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Meru Imekabidhi Hundi yenye  thamani ya Milioni 93 kwa vikundi 26 vya Wanawake,Vikundi 6 vya Vijana na kikundi kimoja cha watu wenye ulemavu.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango amempongeza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Mkurugenzi Mtendaji, Mhe.Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Waheshimiwa Madiwani na wataalamu kwa usimamizi mzuri wa Halmashauri , kuhakikisha inatoa mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu Ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Aidha, Ruyango amevitaka vikundi hivyo 33 vilivyopokea Mkopo kuhakikisha vinatumia mkopo kama ilivyokusudiwa kwa Kujiletea maendeleo kupitia Mkopo huo.

Dkt.John D. Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ametoa wito kwa Wafanyabiashara kulipa tozo mbalimbali za Halmashauri kwani fedha hizo hutumika Kuleta maendeleo Jimboni humo,ikiwa ni ujenzi wa Miradi sambamba na kutenga asilimia 10% kuwawezesha kiuchumi Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu.

Mwl.Zainabu Makwinya ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amewahakikishia Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kuwa Halmashauri hiyo itaendelea kutoa asilimia 10% za makusanyo yake kwa vikundi hivyo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama (CCM) kilichounda Serikali, Sura ya Pili ibara 23.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili amesema Madiwani wa Halmashauri hiyo wamejipanga vyema kuhakikisha utoaji wa mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu unafanyika katika Kata zote 26 kwa kuhamasisha Wananchi na kuwaelimisha juu ya mikopo hiyo.

Aidha Kishili ametoa Wito kwa vikundi vinavyolegalega kurejesha mikopo hiyo kuhakikisha vinarejesha kwa wakati, Ili viendelee kunufaika ikiwa ni pamoja na kuongezewa kiasi Cha mkopo sambamba na kuwezesha Wananchi Wengine kunufaika.

Naye Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya kichama Meru Ndg.Joshua Mbwana amepongeza utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Vitengo katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru unaolenga kukwamua kiuchumi mwananchi wa Meru.

Mwakilishishi wa UWT,ambaye pia ni Diwani Viti maalum Makiba Mhe.Upendo Salumu ametoa Wito kwa Wanawake kuendelea kuilinda sifa ya mwanamke ya uaminifu kwa kuhakikisha mikopo wanayoipata wanaituma kwa lengo kusudiwa na kurejesha kwa Wakati.

Miongoni kwa Wanufaika wameishukuru Serikali kwa kuweka mazingira nafuu na mepesi ya kuwawezesha Wananchi kiuchumi kwani mikopo hiyo imewawezesha kuongeza Mtaji kupata mahitaji yao ya kilasiku nk.


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango wakati wa hafla ya utoaji mikopo.

Dkt.John D. Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki wakati wa hafla ya utoaji mikopo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili  wakati wa hafla ya utoaji Mikopo

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya wakati wa hafla ya ugawaji mkopo.

Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya kichama Meru Ndg.Joshua Mbwana wakati wa hafla ya utoaji mikopo.

Mwakilishishi wa UWT ambaye pia ni Diwani Viti maalum, Makiba Mhe.Upendo Salumu wakati wa hafla ya utoaji mikopo

wanavikundi Wanufaika wa mikopo isiyo na riba, wakati wa hafla ya utoaji mikopo Shilingi Milioni 93.





Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa