• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Jamii yaaswa kutunza mazingira.

Imewekwa: June 5th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Meru imefanya kongamano la wadau wa mazingira ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya  siku ya mazingira duniani   ambapo kitaifa imefanyika jijini Dodoma na  mgeni rasmi ni Mhe.Kassim Majaliwa, waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungana wa Tanzania.



Mgeni Rasmi wa  kongamano hilo  Mhe.Lucas  Kaaya diwani wa Kata ya King'ori na  Mwenyekiti wa kamati ya uchumi ,ujenzi na mazingira ametoa wito kwa jamii, kila mmoja kutambua ni mdau wa mazingira na anawajibu wa kuhakikisha mazingira yanakuwa salama muda wote kwani hakuna maisha bila mazingira salama "mazingira yaliyohifadhiwa ndio uchumi wa taifa, nitoe wito kwa watendaji wa serikali na wananchi kutimiza wajibu wao kutunza mazingira kwa kutii sheria za mazingira na kutoharibu ikolojia" amehimiza Mhe.kaaya


Nao wadau wa mazingira wametoa elimu juu ya umuhimu wa kutunza mazingira sambamba na madhara ya plastiki  ambapo Mtafiti Erick Kato kutoka Taasisi ya Nelson Mandela  amesema mbali na jitihada za serikali kudhibiti madhara ya matumizi ya plastiki kwa kupiga marufuku matumizi ya mifuko,  bado nguvu  zaidi inahitajika katika kudhibiti matumizi ya plastiki inayoleta madhara ardhini, kwa wanyama ,binadamu na hewa kwa ujumla.


Aidha. Mtafiti Kato amesema madhara ya plastiki ndogondogo (microplastics) kwa Binadamu   ni pamoja na kuathiri mfumo wa uzazi na hewa ambapo amebainisha  plastiki huingia kwa binadamu kupitia mbogamboga , viazi ,karoti pamoja na kutumia vyombo vya plastiki kuweka vyakula vya moto nk. Aliongeza kwamba bado elimu ya uelewa juu ya microplastics inahitajika sana kwa jamii na kuwaomba wadau kubuni njia mbadala ya matumizi ya plastiki na kusambaza elimu zaidi juu ya madhara ya plastiki hasa zile ndogo microplastics.


Lewis Nzali ambaye ni

Meneja wa  Baraza la mazingira (NEMC ) kanda ya kaskazini,  ametoa wito kwa jamii kutumia fursa ya taka ni pesa  kuchakata taka kuzaliza bidhaa rafiki kwa mazingira " nitoe wito kwa jamii kutenganisha taka ili kurahisisha matumizi yake kwani taka za mabaki ya chakula hutumika kutengeneza mboji pia taka za  plastiki huchakata kutengeneza bidhaa kama viti/  benchi za  kupumzika hivyo kupunguza  uharibifu wa mazingira"ameeleza Nzali


Mhandisi Arafa Magidi ambae ni mkuu wa kitengo cha mazingira  Bonde la Pangani ametoa wito kwa jamii kuishi kwenye Kauli mbiu ya mwaka huu  ya siku ya Mazingira duniani  "Tanzania ni moja tu,tunza Mazingira " ambapo amebainisha  watanzania wanapaswa kutunza vyanzo vya maji vilivyopo tanzania kwani hakuna namna ya kuchukua vyanzo  kwenye sayari nyingine.


Enock Chengula kutoka  Kijani Pamoja ametoa wito kwa jamii kushiriki kutunza mazingira kwa kupanda miti ambapo wao  Kijani Pamoja katika kufanikisha hilo wameanzisha programu ya kuhamasisha  jamii  kupanda miti , ambapo hulipa Shilingi mia nne kwa kila mti mtu atakaoupanda na kuutunza ndani ya miezi mitatu "tunakupa Mche unautunza ndani ya miezi mitatu tunakulipa shilingi mia nne, kigezo kikubwa ni mti ukue "amefafanua Chengula.


Mkuu wa Idara ya Usafi na mazinga halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Charles Makama ametoa wito kwa wadau kutoa elimu kwa jamii ili kuwa na ushiriki wa pamoja katika kutunza mazingira.


Naye Afisa Maliasi na utalii halmashauri ya Meru Ndg. Charles Mungure amesema Halmashauri hiyo imeweka mikakati ya kutunza mazingira kwa kudhibiti  ukataji miti hovyo  ambapo uongozi wa Kijiji  unakuwa mstari wa mbele kudhibiti hilo kwani  ili mwananchi apate  kibali cha kukata mti kutoka Halmashauri anakuwa na mhutasari wa kikao cha kijiji kilichoridhia.


Mhamasishaji na mdau wa mazingira Ndg.Vicent Uhenga toka VOYOTA  amesema wao huhamasisha jamii wakati wa kusherekea siku za kuzaliwa kupanda idadi ya  miti inayolingana na umri wanaotimiza. Pia ametoa rai miti ya asili kizingatiwa katika mazoezi ya   kupanda miti  .


Dkt. Aman Sanga ambaye amemwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo  amewashukuru  wadau wote walioshiriki    maadhimisho hayo  ya wiki ya mazingira  ikiwa ni pamoja na Baraza la Taifa la uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kaskazini ,Bodi ya Maji Bonde la Pangani, Taasisi ya Sayansi na  Teknolojia ya  Nelson Mandela, ANAPA,TICD, Jobopportunity  Change for future, Dunia Salama Foundation, Twice Foundation, Awe College, Twice Foundation na Ngarasero Mountain lodge.Change for future,Hakiki ndoto zako Organizaton,Kisali na Seu Tv,Usa -River Malihai club,Kijani Pamoja,Dunia Salama Foundation,Duluti Green foundation,Trial Tabzanis,ECH East Africa,Zumbi Family,Kilimanjaro Expert,Mojifa (ECA) na Kwalenawe Cultural

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa