Afisa ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Meru Bi. Restituta Mvungi ikiwa ni siku ya Mtoto Afrika ametoa wito kwa jamii kuwa mstari wa mbele kulinda na kutetea maslahi mapana ya watoto ikiwa ni pamoja na kuwatimizia mahitaji yao pamoja na kutenga muda wa kuwasikiliza.
Restituta ametoa wito huo wakati wa mdahalo wa haki za Mtoto uliofanyika kituo cha Watoto (Watoto Foundation ) ambapo Halmashauri kwa kushirikiana na shirika la Voice of Youth Tanzania (VOYOTA) imetoa elimu sambamba na vifaa vya kujikinga na maambukizi ya COVID 19.
Mkurugenzi wa Shirika la Voice of Youth Tanzania Ndg. Vicent Huega ametoa wito kwa jamii kuendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa wa COVID 19 kwa kunawa mikono na maji tiririka na sabuni na kuzingatia maelekezo ya kujikinga yanayotolewa na Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto .
Wadau wa makao ya kulelea watoto (Watoto Foundation ) wameishukuru Serikali kushirikiana na shirika la VOYOTA kuongoza mjadala huo wa elimuu juu ya haki za Mtoto na wajibu wa jamii sambam ba na utoaji wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya COVID 19.
Aidha Mkurugenzi wa makao ya Watoto Foundation Ndg. Noud V. Hout ametoa wito kwa jamii kutoa malezi kwa watoto na hasa kuwapatia mahitaji Yao ya Msingi ili wasihangaike kutoroka nyumbani kwenda kutafuta huduma na malezi mtaani.
Aidha ,shirika limekabidhi vifaa ambavyo ni ndoo na sabuni kwaajili ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa COVID 19.
BAADHI YA PICHA ZA TUKIO.
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa