• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

JAMII YATAKIWA KUWASAIDIA KINAMAMA KUNYONYESHA WATOTO WACHANGA MAZIWA YAO PEKEE KWA MIEZI 6 YA MWANZO.

Imewekwa: August 7th, 2019


Jamii imehimizwa kuwasaidia kina mama kuwanyonyesha watoto wachanga maziwa yao pekee bila kuwapa vyakula vingine  kwa kipindi cha miezi 6 ya mwanzo kwani maziwa ya mama yanavirutubisho muhimu ambavyo humkinga  mtoto  dhidi ya magonjwa hatarishi kama vile kuhara , magonjwa  ya hewa na maskio.Pia maziwa ya mama ni kinywaji na chakula kinacho msaidia mtoto kukuwa vizuri kimwili na kiakili,hayo yamejiri katika Kilele cha maadhimisho ya wilki ya onyonyeshaji katika  Halmashauri ya Meru, Wilayani Arumeru yaliyofanyika Hospitali ya Wilaya .

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt.Maneno Focus amesema maziwa ya mama ni muhimu sana kwani  huwa na protini zote, vichochezi vya ukuzi, mafuta, wanga, vimeng’enya na vitamini ambavyo ni muhimu kwa ukuzi wenye afya wa Mtoto mchanga  katika miezi ya kwanza ya maisha hivyo amewahimiza kina mama kunyonyesha watoto maziwa yao pekee kwa miezi 6 na pale wanapofika umri kuanzia miezi 7 mbali na kuwa mtoto anaweza tumia vyakula vya lishe wanatakiwa kuendelea kuwanyonyosha hadi wafike umri wa miaka miwili  kwakuwa katika kipindi hicho ndipo ubongo wa mtoto hujitengeneza.

Aidha Dkt.Maneno ametoa rai kwa jamii  kuwasaidia kina mama kunyonyesha maziwa yao pekee miezi 6 ya mwanzo kwa kuacha dhana ya  kuamini mtoto hashibi maziwa ya mama bali kuwajengea mazingira ya kupata maziwa ya kutosha kwa kuwapa lishe stahili pamoja na faraja ili kumwondolea msongo wa mawazo.

Aidha Dkt.Maneno amehitimisha kwa kufafanua kuwa iwapo jamii itashiriki kikamilifu kumsaidia mama kunyonyesha miezi 6 ya mwazo itasaidia kupunguza na kumaliza lishe duni kwa mtoto kwani takwimu zinaonyesha hali ya udumavu  Mkoani  Arusha ni asilimia 25.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Meru Dkt.Maneno Focus akizungumza wakati wa kilele cha Wiki ya unyonyoshaji.

Familia yaBw.Daniel Eliasi 

Kinamama wakifuatilia mafunzo ya unyonyeshaji.

Afisa Lishe Halmashauri ya Meru Asia Ijumaa,amesema kunafaida wapatazo kinamama wanaonyonyesha kwani kwa asilimia kubwa kunyonyesha hupunguza kupata ugonjwa wa saratani ya matiti  pia humsaidia mama kurejea kwenye maumbile yake ya awali kabla ya kupata ujauzito.

Kinamama wakipata elimu juu ya unyonyeshaji maziwa ya Mama.

Afisa Lishe akijibu swali la Mama alihoji nini kifanyike endapo mama hana maziwa ya kutosha? Swali hili limejibiwa endapo itatoke mama anachangamoto ya kunyonyesha afike katika kituo cha Afya kilichopo karibu ili apewe huduma na ushauri wa kitaalamna 

Ndg.Daniel Elias ameeleza yeye humsindikiza mkewe kwani ni jukumu lao wote kumlea mtoto,pia ni faraja kwa Mama na humfanya mtoto kuhisi anapendwa na wazazi wote.


Katika Kilele cha Maadhimisho yaWiki ya unyonyeshaji elimu imetolewa  juu ya unyonyeshaji maziwa ya mama,ulaji bora wa vyakula  pamoja na upimaji magonjwa yasiyoambukiza na ushauri wa kitaalamu umetolewa katika viguo vyote vya Afya vya Halmashaur ya Meru.



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa