• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HALMASHAURI KUU YA CCM WILAYA YA KICHAMA MERU YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA SERIKALI.

Imewekwa: February 6th, 2020

Halmashauri ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kichama Meru imepongeza namna Serikali ilivyowaletea maendeleo wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ikiwa ni utekelezaji wa  ya Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015.

Akizungumza wakati wa Mkutano huo ,Katibu wa CCM Wilaya ya kichama Meru Ndg. Gurisha Mfanga amesema Chama cha Mapinduzi kipo imara na kinaendelea kuisimamia Serikali kuwaletea wananchi maendeleo  ambayo yamefanyika Meru  na yanaendelea kufanyika na kuwavutia zaidi Wananchi na viongozi mbalimbali kuendelea kuiamini CCM  chini ya uongozi makini wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema Serikali chini ya uongozi makini wa  Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli, imeboresha Sekta ya elimu kwa kwa kutoa zaidi ya Milioni 100 kwaajili ya elimu bila Ada kila mwezi katika  Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Muro amesema Serikali  imeboresha Miundombinu ya madarasa,nyumba za walimu na maabara za kujifunzia masomo ya sayansi hivyo kuwezesha Halmashauri hiyo kufanya vizuri kwa kushika nafasi ya tatu Kitaifa na nafasu ya kwanza kimkoa katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne na kidato cha pili kwa mwaka 2019. 

Aidha,Muro amewaeleza Wajumbe wa Halmashauri ya CCM Wilaya kuwa Shule ya Sekondari Kisimiri uliyopo Meru imeshika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2019.

Akihitimisha Muro amesema  katika Sekta ya afya Serikali imesogeza huduma karibu na wananchi kwa kutoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujezi ujenzi na ukarabati wa kituo cha afya Usa -River ambacho  kwa sasa huduma mbali mbali zinatolewa ikiwemo  ya upasuaji .
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel J. Mkongo amesema Halmashauri hiyo kupitia wataalamu wake itaendelea kutekeleza shughuli za  Serikali kwa uadilifu na kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais inayolenga  kuwaletea  maendeleo wananchi hususani wanyonge.


Aidha, Mkutano huo wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya kichama Meru  umefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambapo umeridhia utekelezaji wa ilani ya CCM  katika Wilaya ya Kichama ya Meru .

Katibu wa CCM Wilaya ya kichama Meru Ndg. Gurisha Mfanga.

Wajumbe wa Halmashauri  ya CCM Wilaya ya Kichama ya Meru.

Katibu wa CCM Wilaya ya kichama Meru Ndg. Gurisha Mfanga.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ,Jerry Muro akisoma ilani ya chama cha mapinduzi CCM 

Wajumbe wa Halmashauri ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kichama Meru wakati wa Mkutano.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ,Jerry Muro.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel J. Mkongo akizungumza wakati wa Halmashauri kuu ya CCM.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel J. Mkongo 

Wajumbe wa Halmashauri ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kichama Meru wakati wa Mkutano.

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya ya Meru.

Mkuu wa  Idara ya Utawala na rasilimali watu Halmashauri ya Wilaya ya Meru.





Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa