• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO YAFANYA ZIARA KATIKA MRADI WA CHUO CHA VETA KATA YA UWIRO

Imewekwa: October 18th, 2023

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Mradi wa Ujenzi wa Chuo cha Ufundi stadi (Veta) kinachojengwa Kata ya Uwiro Katika Halmashauri ya Meru.

Ziara hiyo ni utaratibu wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango kukagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri kwa kila robo Mwaka, ambapo ukaguzi huu ni wa robo ya kwanza Kipindi cha Mwezi Julai- Septemba 2023 kwa mwaka wa Fedha 2023/2024.

Ukaguzi huo umehusisha Wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambapo kwa pamoja wamekagua Mradi huo unaojengwa kwa mfumo wa "Force Account" kupitia Kamati tatu za Chuo Cha Ualimu Patandi chini ya Usimamizi wa Mhandisi Mshauri Mponjoli Zakaria kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi Dar- es- Salaam (ARU).

Mradi wa Ujenzi wa chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Katika Kata Uwiro ni moja kati ya utekelezaji miradi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia ambapo Serikali ya Awamu ya Sita ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imekusudia kujenga Vyuo vya Ufundi stadi 63 vya Wilaya na Kimoja cha Mkoa.

Mkuu Wa Chuo cha Ualimu Elimu Maalum Patandi Lucian E. Segesela Katika taarifa yake ameeleza kuwa Serikali imepanga kutekeleza Mradi huo kwa awamu mbili kwa kujenga majengo kumi na nane ambapo tisa yatajengwa sasa na mengine yatajengwa awamu ya pili.

" Kwa sasa majengo yanayojengwa ni Jengo la Utawala, Majengo 3 ya Karakana, jengo la nyumba ya Mkuu wa Chuo, Jengo la madarasa, jengo la choo, jengo la kibanda cha Mlinzi na Jengo la kupokelea umeme.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe. Jeremia Kishili na Wajumbe wa Kamati ya Fedha kwa niaba ya Baraza la Halmashauri wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa ya ujenzi wa chuo cha ufundi stadi (VETA) katika Halmashauri ya Meru.

Hata hivyo, Mhe. Godson Majola Mjumbe wa Kamati hiyo ametoa angalizo kuwa, Kamati za ujenzi ziongeze umakini katika kusimamia ujenzi wa Chuo hicho ikiwa ni pamoja na kuweka nyaraka zote za mradi.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa