• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KATIBU MKUU TAMISEMI ARIDHISHWA NA MIRADI YA EP4R ARUMERU.

Imewekwa: September 14th, 2019

Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Eng.Joseph Nyamhanga, alipotembelea mradi  wa Chumba cha  darasa  Katika Shule ya Msingi Ndoombo Halmashauri ya Meru  Wilayani  Arumeru ambao umekamilishwa kwa  fedha  za mradi wa lipa kulingana na matokeo EP4R, amesema Serikali  kwa Mwaka wa fedha 2018/2019 imetoa Bilioni 65.4 kwaajili ya ujenzi na ukamilishaji wa miundombinu  ya elimu Nchini ambapo Bilioni 29.9 zilitolewa kukamilisha miundombinu Shule za Sekondari na Bilioni 35.5 zilitolewa kukamilisha miundombinu  shule za Msingi, pia imetoa Bilioni 288.485 kwaajili ya Elimu bure ili kuhakikisha watoto watoto wote wa kitanzaniawenye umri wa   kwenda shule wanakwenda  bila Kero ya ada na kudaiwa michango.

Aidha Eng.Joseph Nyamhanga, ameridhishwa na ubora wa ujenzi wa darasa hilo katika shule ya Msingi Ndoombo  uliokamilishwa kwa milioni  12.5 fedha toka Serikalini za programu wa EP4R  ambao nguvu za wananchi na mchango wa Halmashauri ulifikisha Darasa hilo  hatua ya Lenta , amepongeza ufuatiliaji na usimamizi wa fedha za Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu Wilayani hapo.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meru,Emmanuel Mkongo ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano kwa kuboresha Miundombinu ya Elimu katika Halmashauri hiyo kwani mwaka wa fedha 2018/2019 imepokea Zaidi ya milioni 300 kwaajili ya ujenzi wa vyumba 4 vya madasa,matundu 12 ya choo katika Shule za Msingi Tanzanite na Kisimiri juu na ukamilishaji wa  maboma 16(vyumba vya madarasa )katika shule 16 za Msingi sambamba na utoaji wa fedha za Elimu bila malipo kila mwezi, ambapo Halmashauri hiyo hupokea Zaidi ya milioni 60 kugharimia elimu bure kwa shule za Sekondari pia hupokea zaidi ya milioni 55 kwaajili ya Elimu bure shule za Msingi.

Mkongo ameeleza Elimu bure imeleta  mafanikio makubwa katika Halmashauri, kwani kunaongezeko kubwa la  idadi ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza na Darsa la awali ,mwaka 2015 wanafunzi waliojiunga na kidato cha kwanza walikuwa 2622 na 2018 wakawa 4484, pia 2015 waliojiunga na darasa la awali walikua 6809 na 2019 ni 7700.           

Mkongo amesema  kwa kiasi kikubwa Elimu bure imeongeza ufaulu  ambapo matokeo ya kuhitimu elimu ya msingi darasa la saba ( vii ) mwaka 2015  asilimia ya ufaulu ilikua 67.6% na 2018 ikawa 86.6%,pia katika mtiani wa Kuhitimu kidato cha nne mwaka 2015 asilimia ya ufaulu ilikua 95.7% na mwaka 2019 ni 99.4% .

Katibu mkuu Eng.Joseph Nyamhanga,anaendelea na ziara yake Katika Wilaya ya Monduli MKoani Arusha.

Katibu mkuu ofis ya Rais TaAMISEM akizungumza  ndani ya chumba cha darasa Shule ya Msingi Ndoombo kilichokamilishwa kwa fedha za P4R milioni 12.5

Katibu Mkuu ofisi ya Raisi TAMISEM akizungumza baada ya kukagua chumba cha Darasa Shule ya Msingi Ndoombo.


Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Ziara.


Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Ziara

Vyumba vya Madarasa vilivyoboresha kupitia programu ya EP4R shule ya Msingi Tanzanite.

Matundu ya Choo shule ya Msingi Tanzanite 

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa