• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KILELE CHA MASHINDANO YA KUKUZA STADI ZA KKK.

Imewekwa: October 10th, 2019

Kilele cha Mashindano ya kukuza stadi za KKK ,yaani kusoma ,kuandika,kuhesbu, kuchora na utambuzi wa Mwalimu Mahiri katika utengenezaji zana za kufundishia na kujifunzia kwa shule zote za Msingi yamefanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa kushiriksha Walimu watano toka shule za kawaida na walimu watano toka shule zenye vitengo vya elimu maalumu, wanafunzi 40 toka shule za kawaida na wanafunzi 10 toka shule zenye vitengo vya Elimu maalumu.

Afisa Taaluma Msingi Halmashauri Wilaya ya Meru ,Mwl.Enock Sangova amesema Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha wanafunzi wote wanaoingia darasa la tatu wanajua kusoma kuandika na kuhesabu,ambapo ilitoa mafunzo endelevu ya kuwajengea uwezo walimu wa madarasa ya awali ,darasa la kwanza na la pili Nchi Nzima kwa awamu.Katika kuendeleza mafunzo hayo, Ofisi ya Rais TAMISEMI imeanzisha mashindano ya kukuza stadi za KKK yaani kusoma ,kuandika,kuhesbu, kuchora na utambuzi wa Mwalimu Mahiri katika utengenezaji zana za kufundishia na kujifunzia kwa shule zote za Msingi za Serikali Tanzania Bara yakiwa na lengo tajwa hapo juu.

Aidha kilele cha mashindano hayo ni baada ya kufanyika mashindano ngazi za Shule ,Kata ,na Klasta kuanzia 16 Septemba 2019 hadi tarehe 02 Octoba 2019 kwa kushindanisha walimu mahiri na wanafunzi katika ngazi tajwa.

Akifungua Mashindano hayo yaliyoshirikisha Klasta 5 Leganga, Kikatiti, Ngarenanyuki ,Leguruki na Mbuguni, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri Grace Solomoni ambaye ni mkuu wa Idara ya Kilimo ,Ushirika na Umwagiliaji amewapongeza walimu kwa namna wanavyowajibika kwa kujituma na kufanikisha utoaji wa elimu bora .

Naye   Mwenyekiti wa jopo la waamuzi wa mashindano hayo ambaye pia Mthibiti Mkuu wa ubora Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Onesmo Oletaipa wakati wa kutangaza matokeo, amewapo ngeza Walimu na wanafunzi walioshiriki mashindano hayo kwani wameonesha umahiri mkubwa,pia ameeleza katika Halmashauri ya Meru ongezeko nikubwa  la wanafunzi wanaojua Kusoma ,Kuandika na Kuhesabu KKK kwa wastani wa asilimia 97%.

Mwl Oletaipa amemtangaza Mwl Neema Kaya toka Shule ya msingi Tuvaila kuwa ni mshindi wa kwanza nafasi ya mwalimu mahiri kwa shule za kawaida, akifuatiwa na Mwl.Nangaiwa Mmbugu toka shule ya msingi Usariver, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Mwl Mwanaidi Juma toka shule ya Mwakeny.

Kwa upande wa Shule zenye vitengo vya elimu maalumu Mwl Agnes Kimaro toka shule ya Elimu maalum Patandi kitengo cha wasioona aliibuka mshindi wa kwanza nafasi ya mwalimu mahiri, akifuatiwa na Mwl.Rosemary Killenga toka shule ya Msingi Chemchem kitengo cha elimu maalumu kitengo cha ulemavu wa akili huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Mwl.Anna Shayo toka Shule ya Msingi Elimu maalum Patandi kitengo cha Viziwi.

Matokeo ya Wanafunzi wa darasa la kwanza shule za kawaida, Naomi Paulo toka shule ya Nkoanrua, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuhesabu, Mwanafunzi  Rodney William toka shule ya Ambureni, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuandika, Mwanafunzi  Alpha Evarist toka shule ya Chemchem, Klasta ya Kikatiti aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuchora na Mwanafunzi Faith Lain toka shule ya Maasai Vision, Klasta ya Ngarenanyuki aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma.

Kwa upande wa wanafunzi wa kawaida darasa la pili, Mwanafunzi Glory Zakayo toka shule ya Ulong’a, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuhesabu, Mwanafunzi  Dorini Mkonyi toka shule ya Ngyeku, Klasta ya Kikatiti aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuandika, Mwanafunzi  Nancy Elisante toka shule ya Tengeru, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuchora, na Mwanafunzi Innocent Kumbuael toka shule ya Nkoanrua, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma.

Kwa upande wa wanafunzi wenye uhitaji maalum darasa la kwanza, Mwanafunzi Kelvine Mathias  toka shule ya Patandi, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuhesabu na Kuandika kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia, Mwanafunzi Rehema Msitiri  toka shule ya Patandi, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma na Kuchora kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia, Mwanafunzi Harison Emmanuel  toka shule ya Patandi, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma na Kuandika kwa wanafunzi wenye ulemavu wa uoni hafifu na  Mwanafunzi Hashimu Abdi  toka shule ya Tuvaila, Klasta ya Kikatiti aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma kwa wanafunzi wenye ulemavu wa akili.

Kwa upande wa wanafunzi wenye uhitaji maalum darasa la pili, Mwanafunzi Hagai Benedict  toka shule ya Patandi, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kuhesabu na Kuandika kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia na Mwanafunzi Ian Sirikiael  toka shule ya Patandi, Klasta ya Leganga aliibuka mshindi katika mahiri ya Kusoma na Kuchora kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia.

Katika mashindano hayo yaliyoshirikisha Klasta tano, Klasta iliyoibuka kidedea na kupata ushindi wa jumla ni Klasta ya Leganga.

BAADHI YA PICHA ZA TUKIO.

 Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri Grace Solomoni ambaye ni mkuu wa Idara ya Kilimo ,Ushirika na Umwagiliaji akizungu wakati wa wa kilele cha mashindano ya kukuza stadi za KKK.

Walimu na wanafunzi wakati wa ufunguzi wa Kilele cha Mashindano ya kukuza stadi za KKK.

Mwalimu wa elimu Maalumu akitumia lugha ya alama wakati wa ufunguzi Kilele cha Mashindano ya kukuza stadi za KKK.

 Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri Grace Solomoni ambaye ni mkuu wa Idara ya Kilimo ,Ushirika na Umwagiliaji akipokea maelezo toka kwa ,Mwl.Anna Shayo toka Shule ya Msingi Elimu maalum Patandi kitengo cha Viziwi wakati wa kilele cha mashindano ya kukuza stadi za KKK.

Mwl.Anna Shayo toka Shule ya Msingi Elimu maalum Patandi kitengo cha Viziwi akieleza maana ya lugha za alama .

Mwl Agnes Kimaro toka shule ya Elimu maalum Patandi kitengo cha wasioona akielezea matumizi  na maana ya nukta nundu kwa wanafunzi wasiona wakati wa mashindano ya kukuza KKK.

Mwl Agnes Kimaro toka shule ya Elimu maalum Patandi kitengo cha wasioona akielezea matumizi  ya kompyuta maalum kwa wanafunzi wenye uoni hafifu wakati wa mashindano ya kukuza KKK.





Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa