• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KILELE CHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Imewekwa: December 12th, 2023

Na Annamaria Makweba

Maadhimisho ya Kilele cha Siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia yamefanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru huku Mwenyetiki wa UWT Wilaya Julieth Maturo akiwa mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo.

Akizungumza na kundi la wanawake na viongozi mbalimbali katika maadhimisho yaliyofanyika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Muungano, Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa Suala la ukatili wa kijinsia ni janga la Dunia nzima.

“ Ukatili wa kijinsi ni janga la Taifa na Dunia nzima, hivyo sisi kama viongozi iwe ni viongozi wa Chama, Serikali na Dini ni jukumu letu kuhakikisha tunapaza sauti kupinga na kukemea ukatili wa kijinsi katika jamii yetu. Alisema Maturo. 

Aidha, ameeleza kuwa, UWT imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha inapinga masuala yaukatili katika jamii lakini changamoto iliyopo ni wanaofanyiwa ukati li hawatoi ushirikiano ili wahusika wapelekwe kwenye vyombo vya sheria. 

Hata hivyo, Mwanaidi Mahanyu kwa niaba ya Afisa Ustawi Mkoa wa ukatili wa kijinsia ambapo ameelezatoa ufafanuzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambapo ameeleza kuwa siku hizo zimetokana na mfululizo wa matukio ya ukatili yaliyotokea kuanzia tarehe 10 hadi 25 mwezi disemba miaka ya 1960 ambapo wanawake wengi waliuwawa kikatili katika Nchi za Dominika wakiwa katika harakati za kupinga kunyanyaswa. Hii ikapelekea mwaka 1991 kuanzisha siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia.

Sambamba na ufafanuzi huo, Mahanyu ametoa rai kwa wanawake kupambana kutafuta fedha lakini kupambana zaidi kulea familia kwani mwanamke ndiye mlezi mkuu wa familia.

Pia, Katika maadhimisho hayo, Mwenyekiti UWT amezindua Jukwaa la Uwezeshaji wanawake kiuchumi katika Kata ya Usariver.

Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Meru Florah Msilu ameeleza kuwa Uzinduzi wa Majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi ni Agizo la Serikali,hivyo utekelezaji utafanyika kwa Kata zote 26 na hadi Sasa uzinduzi wa majukwaa hayo umefanyika katika Kata 4 ,Kata ya Kikatiti, Akheri, Ambureni na Usariver. Vilevile ameeleza kufikia mwaka 2024 watazindua Jukwaa la Wilaya.

Elimu ya Uchumi imetolewa na maonyesho ya bidhaa mbalimbali za wajasiriamali yamefanyika ili kujikwamua kiuchumi.












Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa