• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KISIMIRI NA KILIMO CHA PARETO

Imewekwa: July 21st, 2021

Wakulima wa zao la pareto katika Kijiji Cha Kisimiri juu Wilayani Arumeru wahamasika kulima zaidi zao la pareto ambalo  hustawi vyema katika kijiji hicho ikiwa ni zao jipya la biashara lisilo hitaji matumizi ya viuatilifu na hutumia mbolea ya samadi .

Godfrey Motika ambaye ni mkulima wa muda mrefu wa zao la pareto amesema zao hilo limemsaidia kujenga nyumba na kuitunza familia yake(poligamy) kwa kipindi chote .

Naye Orneng Irac ambaye ni mkulima wa pareto na Kiongozi wa mila ameiomba Serekali kutengeneza barabara ya kuingia Kijiji hicho kwani ni changamoto kubwa kwenye kilimo cha pareto ambapo imewalazimu wakulima kutumia gharama kubwa ya Usafiri kupeleka  mazao sokoni.

Irac ameliomba Baraza la Pareto Tanzania (PCT) kuongeza idadi ya miche ya pareto inayotolewa kwa wakulima.

Afisa kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Meru Bi. Digna Masawe  amesema zao la kilimo cha  parato ni zao lisilo na gharama kubwa za uzalishaji  kwani mkulima akiwa na Mtaji wa Shilingi  laki 5 anaweza kulima ekari moja na  kupata zaidi  ya milioni nne kwa mchumo wa awamu ndani ya kipindi cha miaka mitatu kwani bei elekezi ya zao hilo ni Tsh.2,600 kwa kilo lakini mkulima anaweza kuuza hadi Tsh.4000 kwa kilo kutoka na ubora .

Masawe amesema Kuna haja ya wakulima wa Kisimiri kulima zaidi zao la pareto ambalo hustawi kwenye mwinuko ambalo ni miongoni kwa mazao ya kimkakati hapa nchin na huchukua muda usiozidi miezi mitatu tuu ili kuanza kuchumwa. 

Afisa kutoka PCT Godluck Tairo amesema zao la pareto linamanufaa kwani Serikali katika kuhakikisha mkulima ananufaika  imeongeza bei ya pareto kutoka Tsh. 2,100 kwa kilo hadi Tsh.2,600 kwa kilo na PCT itahakikisha inato miche kwa wakulima sambamba na kuendelea kuwalipa kwa wakati .

Mhe.Dauson Urio, diwani wa Kata ya Uwiro ametoa wito kwa wananchi wa Kijiji Cha Kisimiri juu kujikita kwenye kilimo cha zao la Pareto ili kujikwamua kiuchumi "rai yangu kwenu kilimo hichi cha  pareto kiitambulishe Kisimiri juu"amehimiza mhe.Urio

Urio amesema Serikali ipo bega kwa bega kuhakikisha changamoto ya barabara inatatuliwa kwani sintofahamu ya ukarabati wa barabara ya kuingia Kijiji hapo imeshatatuliwa na ukarabati  umeanza, pia taarifa yake imetolewaa kwa wakala wa barabara mijini na Vijiji  TARURA .

Mhe.Dauson Urio diwani wa Kata ya Uwiro.

Wananchi wa Kijiji Cha Kisimiri juu wakati wa utoaji elimu ya kilimo cha zao la pareto.

Wananchi wa Kijiji Cha Kisimiri juu wakati wa utoaji elimu ya kilimo cha zao la pareto.

Wananchi wa Kijiji Cha Kisimiri juu wakati wa utoaji elimu ya kilimo cha zao la pareto.

Orneng Irac ambaye ni Kiongozi wa mila na mkulima wa zao la pareto akizungumza wakati wa utoaji elimu ya kilimo cha zao hilo.

Afisa kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Meru Bi.Digna Masawe akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Kisimiri juu.

Afisa kutoka PCT Godluck Tairo akizungumza na Wananchi wa kijiji Cha Kisimiri juu.

Bi.Neema Munisi ,afisa ushirika akitoa elimu juu ya umuhimu wa vyama vya ushirika.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa