• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wanachi Kata ya Maroroni mstari wa mbele kujiletea maendeleo.

Imewekwa: February 19th, 2021

Wananchi wa Kata ya Maroroni ,Halmashauri ya Wilaya ya Meru waendelea kuonyesha jitihada za kizalendo kushiriki kikamilifu katika kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha  huduma za afya sambamba na utoaji elimu bila malipo.

Hayo yamedhihirika katika hafla ya Serikali ya kijiji cha Migandini kilichopo Kata ya Maroronii, kukabidhi  Madawati 27 mapya kwaajili ya wanafunzi wa shule ya Msingi Migandini.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho  Mhe. Christopher Pallangyo amesema wananchi wamehamasika  kushiriki shughuli za maendeleo haswa kwenye sekta ya elimu baada ya Serikali kutoa elimu bila malipo. 

Pallangyo amesema  Serikali ya kijiji hicho katika kuunga mkono utoaji wa elimu bila malipo  imechangia zaidi ya milioni 2 kwa kutumia rasilimali miti na rasilimali watu kutengeneza madawati mapya 27 pamoja na kukarabati madawati 16.

Pallangyo, amesema baada ya kupata taarifa ya uhaba wa madawati katika shule hiyo waliamua kutumia miti ya kijiji kutengeneza mbao na kuwashirikisha  wananchi wenye ujuzi wa ufundi kujitolea kutengeneza madawati hayo  bila malipo.

Pallangyo ameongeza kuwa, Wananchi wa kijiji hicho wamekua mstari wa mbele kushiriki kujiletea maendeleo ambapo kwa kushirikiana na wadau wamefanya ujenzi wa zahanati ya kijiji ambayo imefikia hatua ya lenta, Pia  wamekubaliana kushiriki katika  ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu .


Mwl.David Kyara ambaye ni mwalimu mkuu shule ya Msingi Migandini  amesema shule hiyo yenye wanafunzi 400 ilikuwa na uhaba wa madawati 33, hivyo madawati yaliyokarabati yatapunguza uhaba na kubakiwa madawati 6 ambapo uongozi wa kijiji umeahidi kutengeneza.

Diwani wa Kata ya Maroroni Mhe.Yona Nnko amepongeza utendaji wa mwenyekiti wa kijiji cha Migandini katika gurudumu la kuharakisha  maendeleo sambamba na ushirikiano katika ngazi ya Kata.

Mhe. Yona  amesema anajivuni  wananchi wa Kata hiyo kwani wamekuwa mstari wa mbele katika kujiletea maendeleo,  ambapo jitihada zao ziliungwa mkono na Baraza la Halmashauri hiyo, lililopitisha ujenzi  wa kituo cha afya kitakacho gharimu kiasi cha Sh.Milioni 400 kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo kutekelezwa katika kata hiyo.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Ndg.Exaud Kimaro ambaye pia ni Afisa elimu maalum, amepongeza juhudi za wananchi na uongozi  wa kijiji  hicho na kuahidi kuwasilisha changamoto za uhaba wa vyumba 2 vya madarasa ambavyo wananchi wameshaandaa tofali na mchanga .


Pia Mwl.Kimaro amesema ushiriki  wa wananchi wa Migandini katika maswala ya maendeleo ni wa kuigwa ambapo ametoa wito kwa uongozi wa shule kutunza madawati hayo.


Naye , Afisa elimu Kata Mwl. Juma Msangi amepongeza uongozi wa kijiji cha Migandini na kuhaidi kuendelea kushirikiana na wananchi wa Kata hiyo kuhakikisha wanainua taaluma .

Kulia ni Mwl.Exaud Kimaro akipokea Dawati toka kwa Mhe.diwani wa Kata ya Maroroni na  Mwenyekiyi wa kijiji cha Migangini .

Mwl.Kimaro ambaye amemwakilisha mkurugenzi Wa halmashauri ya Meru akifanya makabidhiano ya madawati kwa uongozi wa shule.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mikandini wakifurahia madawati yaliyotolewa na uongozi wa Kijiji .

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa