• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE YAFANA ARUMERU

Imewekwa: October 30th, 2023

Maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe kwa Mkoa wa Arusha yameadhimishwa leo katika Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri ya Meru yaliyoambatana na huduma mbalimbali za Afya kama upimaji wa hali ya lishe, ulinganisho wa Urefu na Uzito pamoja na kutoa elimu ya vyakula ya Afya na lishe.

Kwa niaba Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John VK. Mongella, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Charles Rashid Mkombachepa ameeleza kuwa dhumuni la maadhimisho hayo ni kuongeza uelewa katika jamii yetu kuhusu umuhimu wa lishe bora wa vijana.

" Lishe bora kwa vijana balehe ni muhimu kwa kipindi cha miaka 10 -19 kwani ni fursa adhimu ya ukuaji na maendeleo ya binadamu baada ya siku elfu moja za mwanzo wa maisha ya mtoto." Alisema Mkombachepa.

Aidha, ameeleza kuwa vijana balehe wana umuhimu wa kuzingatia lishe kwani ndio msingi wa maendeleo ya binadamu na ya Nchi.

Pia, ameeleza kuwa makadirio ya kidunia yanaonyesha kuna vijana Milion 1.2 wenye umri wa miaka 10-19 ambayo inaongezeka kwa kasi kubwa. Kwa Nchi ya Tanzania Vijana balehe wanakadiriwa kuwa robo ya watu wote kwa ujumla.

Mganga Mkuu H/Wilaya ya Meru Dkt. Evarist Chiweka ameeleza kuwa Afya bora ni muhimu kwa nguvu kazi ya Taifa. Pia alieleza madhara ya utapiamlo kwa wanawake na watoto wadogo ambao ndio wahanga wakubwa ambapo ameeleza utapiamlo unasababisha vifo kwa watoto wakati wa kujifungua, Kuzaa mtoto mwenye uzito pungufu na Kuzaa Mtoto ambaye hajafikisha muda wake(Njiti).

Iren Clement Makundi ni mwanafunzi kutoka chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, amefurahi kushiriki katika maadhimisho hayo kwani amejifunza umuhimu wa lishe bora kwa vijana balehe.

" Nimeokolewa na elimu finyu iliyokuwepo katika kichwa changu kwani leo nimeelewa umuhimu wa lishe bora kwa kijana hasa wakati wa kupevuka" Alisema Iren.

Ikumbukwe kuwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 Sura ya 3 Ibara ya 81, imeeleza kuwa huduma za Afya ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya bora ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli za maendeleo ya Nchi.

Siku ya Afya na Lishe kitaifa imefanyika Mkoani Pwani. Kauli Mbiu ya mwaka 2023 ni " Lishe bora kwa Vijana balehe ni chachu ya mafanikio yao"

Dkt. Charles Rashid Mkombachepa akieleza dhumuni la maadhimisho ya siku ya lishe.





Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa