• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MAAFISA 50 WAMEPATIWA MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIRADI YA TASAF MERU.

Imewekwa: August 27th, 2024

Na . Annamaria Makweba

Maafisa wa Serikali wapatao idadi ya 50 katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru wamepatiwa Mafunzo ya  Usimamizi wa Miradi ya TASAF awamu ya III inayotekelezwa katika Halmashauri zote nchini Tanzania.


Mafunzo hayo yamefanyika leo tarehe 27 Agosti 2024 katika ukumbi wa Taasisi ya "The Foundation For Tomorrow(TFFT) na kufunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl. Zainabu J. Makwinya.

Katika Ufunguzi wake, Mkurugenzi Makwinya amewataka Maafisa hao kusikiliza kwa makini na kuelewa kile wanachotakiwa kwenda kufanya ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri kwa miradi itakayoibuliwa na wananchi na siyo kwenda kuwaibulia miradi ya kutekeleza.

"Serikali inatoa mafunzo haya ili muende kuzisaidia jamii katika kuibua Miradi na siyo nyinyi kuwaibulia miradi kwani kwa kufanya hivyo jamii haitakuwa na umiliki wa miradi yao, hivyo lengo kuu ni nyinyi kwenda kuwasimamia ili waibue miradi ambayo kweli itakwenda kutatua changamoto zao.

Mratibu wa TASAF kutoka Makao Makuu Dodoma Bi. Godliver Mvanda ameeleza kuwa lengo la  Mafunzo hayo ni kuwapitisha maafisa hao katika miongozo na kuteua wawezeshaji wanaofahamu mambo yanayohitaji utaalamu ili kuwezesha miradi hiyo kutekelezwa kwa ufanisi unaotakiwa.

Aidha, Bi. Mvanda ameeleza kuwa mpango huu umeandaliwa kwa malengo ya kumwezesha Mlengwa wa TASAF kushiriki katika kuibua miradi lakini pia kushiriki kufanya kazi ambazo zitamwingizia kipato ndani ya siku 60 kwa mwaka watakaofanya kazi hizo kwenye maeneo yao.

Kwa niaba ya Maafisa walioshiriki mafunzo hayo, Afisa Mifugo Merry Kiondo ametoa shukrani kwa Serikali kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo hayo lakini pia ameahidi kuzingatia maelekezo yote yaliyotolewa mafunzo hayo.

Maafisa walioshiriki katika Mafunzo hayo ni pamoja na Maafisa wa Mifugo, Kilimo, Wachumi, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Afya, Elimu Kata, Misitu na Maliasili, Uvuvi, Wahandisi na Umwagiliaji.


fungua hapa kupata video,☝️

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa