• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MAAFISA WAANDIKISHAJI WA TASAF WATAKIWA KUWA WAADILIFU WAKATI WA ZOEZI LA UHAKIKI WA KAYA ZA WANUFAIKA WA TASAF.

Imewekwa: July 13th, 2020

Maafisa wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Meru  watakiwa kuwa waadilifu wakati wa  zoezi la uhakiki wa Kaya za Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (TASAF) katika utekelezaji  wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel J. Mkongo wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo na Wawezeshaji  wa TASAF juu  ya  utekelezaji wa Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF .

Mkongo amewataka wawezeshaji hao kuwa makini wakati wa mafunzo ili kufanikisha zoezi la uhakiki wa kaya za walengwa wa TASAF   na  kuondoa dhana iliyojengeka kwa jamii ya kuwepo Walengwa hewa.

Aidha, Mkurugenzi Mkongo amewataka wawezeshaji hao ambao ni watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuwa waaminifu na waadilifu wakati wa zoezi hilo.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TASAF Bi. Tatu Mwaruka wakati wa hotuba ya ufunguzi, amesema tathimini ya utekelezaji wa kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu ya TASAF imeonyesha kuwa mpango huo umechangia kufikiwa kwa azma ya Serikali ya kupunguza umaskini nchini ambapo umaskini wa mahitaji ya msingi kwa kaya umepungua kwa asilimia 10. Pia  umaskini  uliokithiri umepungua kwa asilimia 12 kwa kaya Maskini sana nchini.

Bi. Tatu ameeleza kuwa Serikali iliamua kuendelea na kipindi cha pili katika awamu ya tatu ya TASAF ili kaya zote zinazoishi katika mazingira duni zipate usaidizi kwani katika kipindi cha kwanza cha TASAF awamu ya tatu,  idadi ya kaya zilizofikiwa ni sawa na 70 % ya Kaya zenye mazingira duni nchini. Hivyo, kipindi cha pili cha TASAF awamu ya tatu kitatekelezwa katika Halmashauri zote 185 Tanzania Bara na Wilaya zote za Zanzibar ambapo jumla ya  kaya milioni moja laki nne na nusu zenye jumla ya watu zaidi ya milioni 7 kote Nchini zitafikiwa ikiwa ni ongezeko la kaya laki tatu na nusu.

Mwakilishi huyo wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF amewatahadharisha wawezeshaji watakao fanya kazi ya uhakiki kuwa  waadilifu  kwani watawajibishwa endapo itabainika uwepo wa Kaya zisizo na sifa katika eneo walilofanya kazi .

Semina hiyo ya kuwajengea uwezo Wawezeshaji wa Halmashauri hiyo inafanyika  kwa siku mbili kuanzia tarehe Julai 13 hadi 14.

Aidha zoezi la kuhakiki Kaya za wanufaika wa TASAF  litaanza tarehe  15 hadi 17 Julai 2020.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Emmanuel J. Mkongo

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TASAF Bi. Tatu Mwaruka

Wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Meru wakati wa Mafunzo.

Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa kikao Kazi.


Wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Meru wakati wa Mafunzo.

Wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Meru wakati wa Mafunzo.

Wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Meru wakati wa Mafunzo.

Wawezeshaji wa TASAF Halmashauri ya Meru wakati wa Mafunzo.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa