• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MADAKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA MENTORSHIP WATAMBULISHWA RASMI HALMASHAURI YA MERU

Imewekwa: October 23rd, 2024

Kambi ya Madaktari Bingwa wa MAMA SAMIA MENTORSHIP PROGRAM wamefika

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru na kukutana na Mhe. Amir Mkalipa pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Meru na kukutana na Mwl. Zainabu J. Makwinya kwa lengo la kuonana na viongozi hao na kutoa mwanga wa namna watakavyofanya kazi ya kutoa huduma ya Afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meru.

Madaktari hao wamewasili katika Hospitali ya Wilaya ya Meru Tarehe  21 Oktoba 2024  na watafanya kazi hadi tarehe  26, Oktoba 2024 kwa kutoa huduma za afya kwa jamii.


Mkuu wa Divisheni ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii  Dkt. Evarist Chiweka ameeleza kuwa Madaktari Bingwa Saba wamefika kwenye kambi hiyo akiwemo daktari bingwa wa magonjwa ya ndani, mfumo wa mkojo na  upasuaji, Daktari bingwa wa Kinywa na Meno, Magonjwa ya akina mama na wanawake, Mtaalam wa Usingizi na gazi na Daktari bingwa wa watoto.

Chiweka ameeleza kuwa madaktari hao watatoa huduma kwa njia ya kliniki maalum na  wagonjwa watapata fursa ya kupata ushauri na matibabu kutoka kwa madaktari bingwa kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Hospitali ya Wilaya Meru.

Aidha, ameeleza kuwa katika Kambi hiyo madaktari watafanya tathmini za afya, upasuaji wa dharura, na wanatoa elimu juu ya afya ya jamii. Walengwa  ni wakazi wa Wilaya ya Meru na maeneo jirani, ambao wana changamoto za kupata huduma bora za afya.

Pia, ameeleza kuwa Huduma zinatolewa kwa ushirikiano na Wizara ya Afya na  lengo ikiwa ni kuboresha upatikanaji wa huduma za afya za kibingwa kwa wananchi na hii ni hatua muhimu katika kuboresha afya ya jamii na kupunguza wingi wa wagonjwa kufuata huduma hizi kwenye Hospital za Rufaa.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE SEMINA YA MAFUNZO YA UCHAGUZI MKUU 2025 October 16, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • DED MERU DC AKABIDHI VYETI KWA TAASISI ZINAZO FANYA VIZURI MERU DC

    August 07, 2025
  • TFS YATOA MSAADA WA MBAO TAKRIBANI MIA 8 HOSPITALI YA WILAYA YA MERU

    August 07, 2025
  • MERU DC YAIBUKA MSHINDI WA PILI MAONYESHO YA NANENANE KANDA YA KASKAZINI

    August 08, 2025
  • UZINDUZI WA JENGO LA TEHAMA SHULE YA SEKONDARI PATANDI MAALUM

    August 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa