• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

BARAZA JIPYA KUWALETEA WANANCHI WA MERU MAENDELEO

Imewekwa: December 16th, 2020

Mheshiwa Jeremia Kishili, Mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Wilayani Arumeru ametoa wito kwa Madiwani wa Halmashauri hiyo kushirikiana ili kuwaletea Maendeleo Wananchi "Wananchi wanahitaji miundombinu mizuri ya barabara, huduma bora za afya na maji hivyo hatuna budi kushirikiana na Mhe.Mbunge, Menejimenti pamoja na wadau kuharakisha maendeleo ya Meru ." amesisitiza Mhe. Kishili.

Hayo yamejiri wakati wa Mkutano wa kwanza wa Baraza jipya la Halmashauri ambapo Waheshimiwa Madiwani 36 wamekula kiapo cha udiwani na kutoa Tamko la Maadili kuanza kazi rasmi.

Kiapo hicho kimeongozwa na Hakimu mkazi wa Mahakama ya mwanzo Maji ya Chai Mhe .Walter Mwijage na kimewajumuisha Madiwani 36 ambapo kati yao madiwani 9
 ni wa Viti Maalumu na mmoja ni Mhe. Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki.

Aidha,  Mhe.Kishili alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kupata kura za wajumbe wote 36. Kwa upande mwingine, Mheshimiwa Felister Nanyaro alichaguliwa kuwa makamu Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kura za ndio za wajumbe wote. Viongozi hawa wamewashukuru wajumbe kwa kuwaamini  na kuahidi kushirikiana nao kuijenga Meru yenye Maendeleo.

Mhe. Dkt.John D. Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki amesema katika kutatua changamoto kubwa ya barabara zisizopitika kirahisi Halmashauri inapaswa kuimirasha usimamizi wa Mitambo yake kwa kuhakikisha shughuli zote za mitambo hiyo zinaratibiwa na Halmashauri yenyewe.

Aidha ,wajumbe walipongeza taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri kwa kipindi ambacho Halmashauri haikuwa na Madiwani. Taarifa hiyo iliwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Emmanuel J. Mkongo .

Aidha, Baraza za Halmashauri lilitekeleza jukumu la uundaji wa Kamati za Kudumu za Halmashauri hiyo kwa kuwachagua Wenyeviti wa Kamati hizo Mheshimiwa Jeremia J. Kishili-Kamati ya Fedha , Utawala na Mipango, Mhe.Lucas Kaaya Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira na  Mhe. Kaanael Ayo Kamati ya Elimu ,Afya na Maji.

Ikumbukwe Waheshimiwa Madiwani wote 35 na Mbunge wanatokana na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Bi. Felister Nanyaro  makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru akila kiapo cha Udiwani.

Mhe. Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki  Dkt.John D. Pallangyo akitoa tamko la maadili (kwa mujibu wa Sheria Mbunge ni diwani katika Baraza la Halmashauri)

Baadhi ya Madiwani wakitoa tamko la Maadili.


Baadhi ya Madiwani wakitoa tamko la Maadili.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Meru Ndg. Emmanuel J. Mkongo  akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kipindi Madiwani hawakuwepo.

Mhe. Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki akishauri kuhusiana na Mitambo ya Halmashauri wakati wa Mkutano.

Waheshimiwa Madiwani wakati wa Mkutano.

Waheshimiwa Madiwani wakati wa Mkutano.

Waheshimiwa Madiwani wakati wa Mkutano.

Baadhi ya viongozi wa CCM  wakati wa Mkutano.


Wakuu wa Idara,na Watumishi wa Halmashauri wakati wa Mkutano.

Wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa Mkutano.

(kulia )Mhe.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru (katikati  )Makamu Mwenyekiti Mhe.Felister Nanyaro ,kushoto ni Mhe.Mbunge John Pallangyo.

Mhe.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru ,Makamu Mwenyekiti Mhe.Felister Nanyaro ,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru.




Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa