• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MAKAMU WA RAIS ATANGAZA NEEMA KWA WANANCHI WA MERU

Imewekwa: May 18th, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango atangaza neema kwa wananchi  wa Meru, ambapo amesema Serikali itatoa magari  matatu zikiwemo  gari mbili za kubebea wagonjwa sambamba na kupanga watumishi  wasiopungua 25 wa  afya wakiwemo madaktari  kwa ajili ya kuwahudumia wananchi katika Halmashauri  ya Wilaya  ya  Meru.


Dkt Mpango amesema  hayo baada ya kuzindua jengo la huduma  za  dharura (EMD) katika Hospitali  ya  Wilaya  ya  Meru Wilayani  Arumeru, ampapo Serikali  ilitoa Milioni 300 za ujenzi  wa jengo hilo na milioni mia 509  za Vifaa tiba zikiwemo mashine za kisasa .


Aidha, Dkt.Mpango ametoa wito kwa watumishi wa afya hususani wa Kitengo  cha huduma za dharura  kuwahudumia wananchi kwa  ufanisi, weledi na kujitoa kwani  mgonjwa  anapokuwa mahututi hupata faraja kwa namna anavyohudumiwa.


Vilevile Dkt. Mpango amewataka watumishi kulinda na kutunza  miundombinu iliyopo kuleta tija zaidi ikiwa ni pamoja na utunzaji wa mazingira ya hospitali na  kudhibiti  ubadhirifu wa  dawa  ili wananchi waweze kunufaika na kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi shupavu wa Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais  wa  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania .


Kuhusu changamoto kubwa ya Barabara  katika Halmashauri  hiyo Dkt.Mpango ameielekeza  Ofisi ya Rais  Tawala  za  Mikoa  na  Serikali  za  Mitaa (TAMISEMI)  kupitia Wakala wa Barabara  Mjini na Vijijini (TARURA) kuona uwezekano wa kukarabati  barabara  za Halmashauri  hiyo .


Awali, Mkuu wa  Wilaya  ya  Arumeru  Mhe.Emmanuela  Kaganda  kwa niaba ya Wananchi  wa Meru amemshukuru  Rais Dkt.Samia  Suluhu  Hassan  na  Serikali  yake kutoa fedha nyingi za maendeleo katika Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Meru  zikiwemo Bilioni 1.9  za  uboreshaji  sekta  ya  Elimu na  Afya, Bilioni 1.6 za kurasimisha ardhi na Milioni 550  fedha za tozo kwa ajili ujenzi wa kituo cha afya Mareu na ukamilishaji wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule za Sekondari  umoja Kingori na Muungano.



Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa