• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MAREU WATUMA SALAAM KWA MHE.RAIS

Imewekwa: January 7th, 2022

Wananchi wa Kijiji cha Mareu, Kata ya King'ori Halmashauri ya Wilaya ya Meru wameishukuru Serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Shilingi Milioni 250 fedha za tozo za miamala ya simu kwaajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kijiji hicho.

Wakizungumza Kwa nyakati tofauti Wananchi hao wameishukuru Serikali kutoa fedha hizo Milioni 250 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya kwenye Kijiji Chao ambapo watapata huduma za afya katika umbali mdogo "tunamshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutoa fedha hizi kwani tulikuwa tunafuata huduma za afya Mkoa wa jirani au katika Hospitali  ya Wilaya iliyopo mbali na kijiji hichi, hivyo niwaombe Watanzania wenzangu tushirikiane katika Kujiletea maendeleo" amesema Janeth

Naye Magdalena amesema  Wanawake wa Kata ya King'ori hawana budi kumshukuru Mhe.Rais kwa ujenzi wa Kituo hicho cha Afya kwani ni wanufaika wakuu hususani katika Swala la kujifungua "tunaishukuru Serikali kupitia fedha za tozo tutajifungulia Sehemu salama na kupata huduma Bora za afya.

Aidha, hayo yamejiri wakati Mhe.Dkt. Godwin Molel Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto alipotembelea Ujenzi wa Kituo hicho cha Afya akiambatana na Mhe.Dkt.John D Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ikiwa ni ziara ya Mhe.Mbunge kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo Jimboni sambamba na kusikiliza na kutatua kero za Wananchi.

Katika Ziara hiyo  iliyowajumuisha Katibu tawala Wilaya ya Arumeru Mwl.Jemsi Mchembe, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili pamoja na wajumbe wa Kamati ya ulinzi na Usalama na  Wataalamu wa Halmashauri ya Meru Vituo vya Afya vilivyotembelewa ni  Mareu, Makiba , Momela na Zahanati ya Songoro.

Maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Kituo cha Afya Mareu ,ujenzi unaogharimu Shilingi Milioni 250  fedha za tozo za miamala ya simu.

Mhe.Dkt. Molel Naibu waziri wa afya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Dkt.John D.Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya na Mhe.Lukas Kaaya Diwani wa Kata ya King'ori wakati Wakizungumza na Wananchi wa Kijiji Cha Mareu.


Mhe.Dkt. Molel Naibu waziri wa afya maendeleo ya Jamii ,Jinsia,wazee na watoto alipotembelea Ujenzi wa Kituo cha Afya Mareu.

Mhe.Dkt. Molel Naibu waziri wa afya maendeleo ya Jamii,Jinsia,wazee na watoto akizungumza na Wananchi  wa kijiji cha Makiba.

Mhe.Dkt.John D Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki akizungumza na Wananchi wa Kata ya Makiba

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mhe.Jeremia Kishili akizungumza na Wananchi wa Kata ya Makiba

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya akizungumza wakati wa ziara ya Mhe.Munge Jimbo la Arumeru Mashariki katika Kata ya Makiba.

Ndg.Hungura Mbwana, Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya Meru akizungumza wakati wa Ziara ya Mhe.Mbunge jimbo la Arumeru Mashariki, ameupongeza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM  kwenye Miradi ya maendeleo .

Wananchi wa Kata ya Makiba wakati wa ziara ya Mhe.Mbunge Jimbo la Arumeru Mashariki.

Mhe.Dkt. Molel Naibu waziri wa afya maendeleo ya Jamii,Jinsia,wazee na watoto akikagua ujenzi wa Jengo la Kituo cha Afya Mareu.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa