• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU MSHINDI WA KWANZA UMITASHUMTA MKOANI ARUSHA

Imewekwa: June 11th, 2018

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wiaya ya Meru Mwl.Sara Kibwana amesema Halmashauri ya Wilaya ya Meru imeibuka mshindi wa kwanza na wa  jumla ngazi ya Mkoa kwenye mashindano  ya Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) yaliyofanyika tarehe 06 Juni 2018 hadi 10 Juni 2018 ambapo Halmashauri 7 za Mkoa wa Arusha zilishiriki .

Mwl.Kibwana amefafanua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Meru imezawadiwa vikombe 5 kutokana na kuwa mshindi wa kwanza kwenye mpira wa miguu wavulana, Mpira wa wavu wasichana, Mpira wa mikono wasichana na Mpira wa kengele  pia ilikuwa mshindi wa pili kwenye mchezo wa mpira wa wavu wavulana.

Mwl.Kibwana amesema siri ya ushindi huo ni pamoja na maandalizi mazuri yaliyofanyika kwani Halmashauri hiyo ilitoa maelekezo  zaidi ya miezi 9 iliyopita kwa Walimu Wakuu  wa Shule za Msingi kuhakikisha kila wiki wanafunzi wanakua nasiku za kufanya  michezo pia maandalizi yalikuwa mazuri wakati wa michezo kwakuwa wachezaji walijiandaa kikamilifu kwa kukaa siku 5 kambini.

 Naye Afisa utamaduni wa Halmashauri  ya Wilaya ya Meru, Senyaeli  Pallangyo amesema uchaguzi wa wachezaji kwa kuzingatia viwango uliofanyika kuanzia ngazi ya chini hadi Wilaya umechangia  ushindi huo mkubwa ikiwa ni pamoja na uwezo wa makocha sambamba na wachezaji  kuwa na nidhamu ya hali ya juu  na kufuata taratibu za michezo .

Jumla ya wachezaji 25 kutoka timu mbalimbali za Halmashauri yaWilaya ya Meru na Makocha 4  wamechaguliwa kuunda timu ya Mkoa wa Arusha .

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa mwaka huu 2018 imekuwa mshindi wa kwanza  na wajumla kwa ngazi ya Mkoa wa Arusha wenye Halmashauri 7 katika mashindano ya michezo ya umoja wa michezo Shule za Sekondari Tanzania ( UMISSETA) na  umoja wa michezo na taaluma shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) na kuzawadiwa jumla ya Makombe ya ushindi 10

vikombe 5 vya ushindi wa Mashindano ya UMITASHUMTA kuwa mshindi wa kwanza kwenye mpira wa miguu wavulana, Mpira wa wavu wasichana, Mpira wa mikono wasichana na Mpira wa kengele  pia ilikuwa mshindi wa pili kwenye mchezo wa mpira wa wavu wavulana.

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru ,wakuu wa Idara/Vitengo pamoja na watumishi wengine wakati wa mapokezi  ya vikombe 5 vya ushindi katika ,mshindi wa kwanza kwenye mpira wa miguu wavulana, Mpira wa wavu wasichana, Mpira wa mikono wasichana na Mpira wa kengele  pia ilikuwa mshindi wa pili kwenye mchezo wa mpira wa wavu wavulana.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • TAHAPAO NA MERU DC WAWEKA NGUVU KWENYE KAMATI ZA MTAKUWA

    February 19, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa