Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango amewaongoza wananchi na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuadhimisha siku ya mashuja kwa kupanda miti kwenye chanzo cha maji Ndurumanga pamoja na kufanya Usafi wa Mazingira .
Mhandisi Ruyango amesititiza mshikamano , amani na uzalendo kwani Mashujaa walijitolea maisha yao kwa ajili ya nchi yetu hivyo wananchi wanawajibu wa kuwa walinzi wa kwanza wa nchi yao kwa kutoa taarifa zitakazo saidia kulinda na kudumisha amani iliyopo.
Aidha Mhe.Ruyango amesema ili shughuli hizi za kijamii zilizofanyika kuwa na tija ni muhimu swala la usafi kuimarishwa kwa kila mwananchi kuhakikisha eneo lake ni safi sambamba na utunzaji wa miti na vyanzo vya maji " nielekezi ili usafi huu kuwa na tija kila ofisi na maeneo ya biashara kuwe na vyombo vya kuhifadhi taka ili kuepuka utupaji hovyo wa taka na uchafuzi wa mazingira"amehimiza Mhandisi Ruyango.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya amesema ni muhimu uzalendo Mkubwa wa mashujaa waliojitolea uhai kwa ajili ya nchi yetu kurithishwa kwa vizazi vijavyo ambapo ushiriki wa wanafunzi mwakani ni muhimu.
Aidha Mwl.Makwinya amesema katika kuwakumbuka mashujaa miche ya miti 200 imepandwa kwenye chanzo cha Maji Ndurumanga pia wadau wa mazingira wa mechangia miche mia nane ambapo ameelekeza wananchi wananchi kuchuku miche ya miti hiyo kwenda kupanda majumbani kama ukumbusho wa mashujaa wetu. Mwl.Makwinya amesema kwa mwaka 2021/2022 zaidi ya miche Milioni 1.5 ilipandwa ndani ya Hlmashauri ya Meru.
Mhe.Jeremi Kishili amewapongeza wananchi na watumishi kushiriki maadhimisho hayo ambapo amehimiza mshikamani.
Madhimidho hayo ya siku ya mashujaa katika Halmashauri ya Meru yamefanyika kwa kupanda miti 200 katika chanzo cha maji Ndurumanga na kufanya Usafi eneo la Halmashauri na maeneo ya kituo cha daladala Leganga
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Anwani: P.o. Box 462 Usa River
Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482
Simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@merudc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa