• Barua pepe |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Meru District Council
Meru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Meru

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu na Ufatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Manunuzi na ugavi
      • Uchaguzi
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Misitu
    • Ufugaji wa Ngombe wa Maziwa
    • Ujenzi wa Kituo cha Biashara
    • Ujenzi wa Eneo la Mapumziko
    • Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Malori cha kisasa
    • Ujenzi wa kituo cha Michezo
    • Kilimo cha Nyanya
    • Ufugaji wa Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • AIDS
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Utaratibu
  • Kituo cha habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MERU WAMSHUKURU MHE.RAIS KUTOA FEDHA UJENZI BWENI LA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM,DED AAGIZA UJENZI KUKAMILIKA KWA WAKATI.

Imewekwa: January 5th, 2022

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya ameagiza ujenzi wa bweni la wanafunzi  wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Patandi  kukamilika kwa wakati na kwa ubora.

Makwinya ametoa agizo hilo wakati akizungumza na kamati za ujenzi wa Mradi huo, Walimu, Viongozi ngazi ya Kata na Vijiji pamoja na fundi, na kuwahimiza kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuharakisha kasi ya ujenzi "Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan anawathamini watoto wenye mahitaji maalum ambapo ametoa fedha hizi Shilingi milioni 80 kuwajengea bweni, hivyo hamna budi kushirikiana na  kusimamia  ujenzi huu ukamilike kwa wakati na kwa viwango "amehimiza Makwinya

Vilevile Mwl.Makwinya amemtaka fundi wa Mradi huo Ndg.Kanankira Somi kuongeza idadi ya vibarua pamoja na mafundi ili kurahisisha ukamilishaji wa Mradi "fundi ukiongeza idadi ya vibarua hauongezi gharama bali  unapunguza siku za kufanya Kazi kwani kazi ambayo ingefanywa na vibarua 5 kwa Siku 10 itafanywa kwa Siku 5  na vibarua 10 "amefafanua Makwinya

Pia.Makwinya amewaagiza wataalam akiwemo  Mhandisi wa ujenzi, Afisa manunuzi  na Mkuu wa Shule hiyo kuhakikisha wanafuatilia ujenzi huo kwa karibu, kukagua na kushauri kwa kila hatua ya ujenzi "Mhandisi wa ujenzi hakikisha fundi anafika eneo mradi kwa wakati na kazi zinafanyika na Afisa manunuzi hakikisha vifaa vinapatikana kwa wakati
" Ameelekeza Makwinya

Naye Mhe.Julius Mungure Diwani wa Kata ya Akheri, unapotekelezwa Mradi huo  bweni hilo ameishukuru serikali ya awamu ya Sita ikiongozwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan  kutambua umuhimu wa kuwajengea fursa na mazingira mazuri ya kusoma watoto wenye mahitaji maalum kwa kutoa Milioni 80 kwaajili ya ujenzi wa bweni.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Patandi Jackline Mtui  amesema ujenzi wa bweni hilo utasaidia usalama kwa watoto sambamba na watoto hao kuhudhuria mafunzo kwani wengi wanaishi mbali na Shule na mara nyingi hushindwa kuhudhuria masomo kutokana na gharama za usafiri .

Aidha,Serikali ya awamu ya Sita ikiongozwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan  imetoa fedha za Kutekeleza miradi mbalimbali inayoendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Milioni 250 fedha za tozo   kujenga  Kituo cha Afya Mareu ,Milioni 300 fedha za UVIKO -19  kujenga Jengo la dharura katika Hospitali ya Wilaya,  Milioni 470 kujenga  Shule mpya ya Sekondari Ambureni ,
Milioni 80  kujenga  bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Patandi.

Pia. Halmashauri kupitia mapato yake ya ndani kwa robo ya kwanza ya mwaka 2021/2022 imetoa Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Maroroni.

Ikumbukwe
Serikali ilitoa Bilioni 1.4 za ujenzi wa Vyumba 70 vya Madarasa katika shule za Sekondari ambapo tarehe 29 Desemba 2021 Madarasa hayo  yalikamilika.

 *Kazi iendelee*

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE USAILI October 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2024
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MTAALA WA ELIMU YA AWALI NA MSINGI 2022. February 18, 2022
  • UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA NGURUDOTO LIMEANZA. November 27, 2018
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO WIKI YA UTYUMISHI WA UMMA 2025 DODOMA

    June 13, 2025
  • AJIRA MPYA MERU DC WAPATIWA MAFUNZO

    April 02, 2025
  • NAIBU WAZIRI MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU AKAGUA MIRADI YA S.O.S

    March 15, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA TAUSI MERU DC YAFUNGWA

    February 15, 2025
  • Tazama Vyote

Video

ELIMU YA KUKABILIANA NA TAHADHARI YA MVUA ZA EL NINO YAANZA KUTOLEWA HALMASHAURI YA MERU.
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • Kupata Salary Slip
  • Sheria ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Meru

Kiungo Kuhusiana

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Utumishi
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Mkoa wa Arusha
  • Ajira Portal
  • Government Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Meru

    Anwani: P.o. Box 462 Usa River

    Simu ya Mezani: (+ 255) 272970482

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@merudc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Meru. Haki zote zimehifadhiwa